Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8

Agano la Kale

Agano Jipya

Wimbo Ulio Bora 3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Usiku nikiwa kitandani mwangu,niliota namtafuta nimpendaye moyoni mwangu;nilimtafuta, lakini sikumpata.

2. Niliamka nikazunguka mjini,barabarani na hata vichochoroni,nikimtafuta yule wangu wa moyo.Nilimtafuta, lakini sikumpata.

3. Walinzi wa mji walinionawalipokuwa wanazunguka mjini.Basi nikawauliza,“Je, mmemwona mpenzi wangu wa moyo?”

4. Mara tu nilipoachana nao,nilimwona mpenzi wangu wa moyo;nikamshika wala sikumwachia aondoke,hadi nilipompeleka nyumbani kwa mama yangu,hadi chumbani kwake yule aliyenizaa.

5. Nawasihini, enyi wanawake wa Yerusalemu,kama walivyo paa au swala,msiyachochee wala kuyaamsha mapenzi,hadi hapo wakati wake utakapofika.

Bibi arusi

Shairi la tatu

6. Ni kitu gani kile kitokacho jangwanikama mnara wa moshi,kinukiacho manemane na ubani,manukato yauzwayo na wafanyabiashara?

7. Tazama! Ni machela ya Solomoni;amebebwa juu ya kiti chake cha enzi;amezungukwa na walinzi sitini,mashujaa bora wa Israeli.

8. Kila mmoja wao ameshika upanga,kila mmoja wao ni hodari wa vita.Kila mmoja ana upanga wake mkononi,tayari kumkabili adui usiku.

9. Mfalme Solomoni alijitengenezea machela,kwa mbao nzuri kutoka Lebanoni.

10. Nguzo zake zilitengenezwa kwa fedha;mgongo wake kwa dhahabu;mahali pa kukalia pamefunikwa vitambaa vya zambarau,walichoshona kwa upendo wanawake wa Yerusalemu,waliokishonea alama za upendo.

11. Njoni basi enyi wanawake wa Siyoni,mkamwone mfalme Solomoni.Amevalia taji aliyovikwa na mama yake,siku alipofanya harusi yake,naam, siku ambayo moyo wake ulijaa furaha.