Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8

Agano la Kale

Agano Jipya

Wimbo Ulio Bora 6 Biblia Habari Njema (BHN)

Wanawake

1. Ewe mwanamke uliye mzuri sana;amekwenda wapi huyo mpenzi wako?Ameelekea wapi mpenzi wakoili tupate kushirikiana nawe katika kumtafuta?

Bibi arusi

2. Mpenzi wangu amekwenda bustanini mwake,mahali ambapo rihani hustawi.Yeye analisha kondoo wakena kukusanya yungiyungi.

3. Mimi ni wake mpenzi wangu, naye ni wangu;yeye huwalisha kondoo wake penye yungiyungi.

Bwana arusi

Shairi la tano

4. Mpenzi wangu, wewe u mzuri kama Tirza,wapendeza kama Yerusalemu,unatisha kama jeshi lenye bendera.

5. Hebu tazama kando tafadhali;ukinitazama nahangaika.Nywele zako ni kama kundi la mbuzi,wateremkao chini ya milima ya Gileadi.

6. Meno yako kama kundi la kondoo majikewanaoteremka baada ya kuogeshwa.Kila mmoja amezaa mapacha,na hakuna yeyote aliyefiwa.

7. Mashavu yako ni kama nusu mbili za komamanga,nyuma ya shela lako.

8. Wapo malkia sitini, masuria themanini,na wasichana wasiohesabika!

9. Hua wangu, mzuri wangu, ni mmoja tu,na ni kipenzi cha mama yake;yeye ni wa pekee kwa mama yake.Wasichana humtazama na kumwita heri,nao malkia na masuria huziimba sifa zake.

10. Nani huyu atazamaye kama pambazuko?Mzuri kama mwezi, mwangavu kama jua,na anatisha kama jeshi lenye bendera.

11. Nimeingia katika bustani ya milozikutazama machipuko ya bondeni,kuona kama mizabibu imechanua,na mikomamanga imechanua maua.

12. Bila kutazamia, mpenzi wangu,akanitia katika gari la mkuu.

Wanawake

13. Rudi, rudi ewe msichana wa Mshulami.Rudi, rudi tupate kukutazama.Mbona mwataka kunitazama miye Mshulamikana kwamba mnatazama ngomakati ya majeshi mawili?