Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8

Agano la Kale

Agano Jipya

Wimbo Ulio Bora 4 Biblia Habari Njema (BHN)

Bwana arusi

1. Hakika u mzuri ewe mpenzi wangu,hakika u mzuri!Macho yako ni kama ya huanyuma ya shela lako,nywele zako ni kama kundi la mbuziwashukao katika milima ya Gileadi.

2. Meno yako ni kama kondoo majike waliokatwa manyoyawanaoteremka baada ya kuogeshwa.Kila mmoja amezaa mapacha,na hakuna yeyote aliyefiwa.

3. Midomo yako ni kama utepe mwekundu,kinywa chako chavutia kweli.Nyuma ya shela lako,mashavu yako ni kama nusu mbili za komamanga.

4. Shingo yako ni kama mnara wa Daudi,uliojengwa ili kuhifadhia silaha,ambako zimetundikwa ngao elfu mojazote zikiwa za mashujaa.

5. Matiti yako ni kama paa mapacha,ambao huchungwa penye yungiyungi.

6. Nitakaa kwenye mlima wa manemane,na kwenye kilima cha ubani,hadi hapo kutakapopambazuka,na giza kutoweka.

7. Tazama ulivyo mzuri ee mpenzi wangu,wewe huna kasoro yoyote.

8. Njoo, bibiarusi wangu tuondoke Lebanoni;na tuiachilie mbali Lebanoni.Shuka toka kilele cha mlima Amana,toka kilele cha Seniri na Hermoni,toka mapango ya simba,toka milima ya chui.

9. Umefurahisha moyo wangu, dada yangu, bi arusi,umefurahisha moyo wangu,kwa kunitupia jicho mara moja tu,na kwa huo mkufu wako shingoni.

10. Dada yangu, bi arusi;pendo lako ni tamu ajabu.Ni bora kuliko divai,marashi yako yanukia kuliko viungo vyote.

11. Midomo yako yadondosha asali, ee bibiarusi wangu;ulimi wako una asali na maziwa.Harufu nzuri ya mavazi yako ni kama ya Lebanoni.

12. Dada yangu, naam, bi arusi,ni bustani iliyofichika,bustani iliyosetiriwa;chemchemi iliyotiwa mhuri.

13. Machipukizi yako ni bustani ya mikomamangapamoja na matunda bora kuliko yote,hina na nardo.

14. Nardo na zafarani, mchai na mdalasinimanemane na udi,na mimea mingineyo yenye harufu nzuri.

15. U chemchemi ya bustani,kisima cha maji yaliyo hai,vijito vitiririkavyo kutoka Lebanoni.

Bibi arusi

16. Vuma, ewe upepo wa kaskazi,njoo, ewe upepo wa kusi;vumeni juu ya bustani yangu,mlijaze anga kwa manukato yake.Mpenzi wangu na aje bustanini mwake,ale matunda yake bora kuliko yote.