Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8

Agano la Kale

Agano Jipya

Wimbo Ulio Bora 7 Biblia Habari Njema (BHN)

Bwana arusi

1. Nyayo zako katika viatu zapendeza sana!Ewe mwanamwali wa kifalme.Mapaja yako ya mviringo ni kama johari,kazi ya msanii hodari.

2. Kitovu chako ni kama bakulilisilokosa divai iliyokolezwa.Tumbo lako ni kama lundo la nganolililozungushiwa yungiyungi kandokando.

3. Matiti yako ni kama paa mapacha,ni kama swala wawili.

4. Shingo yako ni kama mnara wa pembe za ndovu;macho yako ni kama vidimbwi mjini Heshboni,karibu na mlango wa Beth-rabi.Pua yako ni kama mnara wa Lebanoni,ambao unauelekea mji wa Damasko.

5. Kichwa chako juu yako ni kama mlima Karmeli,nywele zako za ukoka zangaa kama zambarau;uzuri wako waweza kumteka hata mfalme.

6. Tazama ulivyo mzuri na wa kuvutia!Ewe mpenzi, mwali upendezaye!

7. Umbo lako lapendeza kama mtende,matiti yako ni kama shada za tende.

8. Nilisema nitaupanda mtende na kuzichuma shada za tende.Kwangu matiti yako ni kama shada za zabibu,harufu nzuri ya pumzi yako ni kama matofaa;

9. na kinywa chako ni kama divai tamu.Basi divai na itiririke hadi kwa mpenzi wangu,ipite juu ya midomo yake na meno yake!

Bibi arusi

10. Mimi ni wake mpenzi wangu,naye anionea sana shauku.

11. Njoo ewe mpenzi wangu, twende mashambani,twende zetu tukalale huko vijijini.

12. Tutaamka mapema, twende kwenye mashamba ya mizabibu,tukaone kama imeanza kuchipua,na kama maua ya zabibu yamekwisha kuchanua,pia kama mikomamanga imeanza kutoa maua.Huko ndiko nitakapokupatia pendo langu.

13. Harufu nzuri ya tunguja imejaa hewanikaribu na milango yetu kuna kila aina ya matunda bora,yote mapya na ya siku za nyuma,ambayo nimekuwekea wewe mpenzi wangu.