Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8

Agano la Kale

Agano Jipya

Wimbo Ulio Bora 1 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Wimbo wa Solomoni ulio bora kuliko nyimbo zote.

Bibi arusi

Shairi la kwanza

2. Heri midomo yako inibusu,maana pendo lako ni bora kuliko divai.

3. Manukato yako yanukia vizuri,na jina lako ni kama marashi yaliyomiminwa.Kwa hiyo wanawake hukupenda!

4. Nichukue, twende zetu haraka,mfalme amenileta katika chumba chake.Tutafurahi na kushangilia kwa sababu yako,tutasifu mapenzi yako kuliko divai.Wanawake wana haki kukupenda!

5. Enyi wanawake wa Yerusalemu,mimi ni mweusi na ninapendeza,kama mahema ya Kedari,kama mapazia ya Solomoni.

6. Msinishangae kwa sababu ni mweusi,maana jua limenichoma.Ndugu zangu walinikasirikia,wakanifanya mlinzi wa mashamba ya mizabibu.Lakini sikutunza shamba langu la mizabibu.

7. Hebu niambie ee wangu wa moyo,utawalisha wapi kondoo wako?Ni wapi watakapopumzikia adhuhuri?Kwa nini mimi nikutafutekati ya makundi ya wenzako?

Bwana arusi

8. Ewe upendezaye kuliko wanawake wote;kama hujui, fanya hivi:Zifuate nyayo za kondoo;basi, walishe mbuzi wako karibu na hema za wachungaji.

9. Wewe ee mpenzi wangu,nakulinganisha na farasi dume wa magari ya Farao.

10. Mashavu yako yavutia kwa vipuli,na shingo yako kwa mikufu ya johari.

11. Lakini tutakufanyizia mikufu ya dhahabu,iliyopambwa barabara kwa fedha.

Bibi arusi

12. Mfalme alipokuwa kwenye kochi lake,marashi yangu ya nardo yalisambaa kila mahali.

13. Mpenzi wangu ni kama mfuko wa manemane kwangu,kati ya matiti yangu.

14. Mpenzi wangu ni kama maua ya hina yachanuayo,kwenye mashamba ya mizabibu huko Engedi.

Bwana arusi

15. Hakika u mzuri, ee mpenzi wangu,hakika u mzuri!Macho yako ni kama ya hua!

Bibi arusi

16. Hakika u mzuri ewe nikupendaye,u mzuri kweli!Majani mabichi yatakuwa kitanda chetu;

17. mierezi itakuwa nguzo za nyumba yetu,na miberoshi itakuwa dari yake.