Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14

Agano la Kale

Agano Jipya

Hosea 6 Biblia Habari Njema (BHN)

Toba isiyo ya kweli

1. “ ‘Twendeni, tukamrudie Mwenyezi-Mungu!Yeye mwenyewe ameturarua,lakini yeye mwenyewe atatuponya.Yeye mwenyewe ametujeruhi,lakini yeye mwenyewe atatibu majeraha yetu.

2. Baada ya siku mbili, atatupa uhai tena,naam, siku ya tatu atatufufuaili tuweze kuishi pamoja naye.

3. Basi tumtambue,tujitahidi kumjua Mwenyezi-Mungu.Kuja kwake ni hakika kama alfajiri,yeye atatujia kama manyunyu,kama mvua za masika ziinyweshayo ardhi.’”

4. Lakini Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Nitakutendea nini ee Efraimu?Nikufanyie nini ee Yuda?Upendo wenu kwangu ni kama ukungu wa asubuhi,kama umande unaotoweka upesi.

5. Ndiyo maana nimewavamia kwa njia ya manabii,nimewaangamiza kwa maneno yangu,hukumu yangu huchomoza kama pambazuko.

6. Maana ninachotaka kwenu ni upendo na si tambiko,Kumjua Mungu na si kutoa sadaka za kuteketezwa.

Uhalifu umeenea kote nchini

7. “Lakini mlilivunja agano langukama mlivyofanya mjini Adamu;huko walinikosea uaminifu.

8. Gileadi ni mji wa waovu,umetapakaa damu.

9. Kama wanyang'anyi wamwoteavyo mtu njiani,ndivyo na makuhani walivyojikusanya na kuvizia.Wanaua watu njiani kuelekea Shekemu,naam, wanatenda uovu kupindukia.

10. Nimeona jambo la kuchukiza sanamiongoni mwa Waisraeli:Watu wa Efraimu wanakimbilia miungu minginenaam, Waisraeli wamejitia unajisi.

11. Nawe Yuda hali kadhalika,nimekupangia wakati utakapovuna adhabu.