Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14

Agano la Kale

Agano Jipya

Hosea 8 Biblia Habari Njema (BHN)

Makosa makuu ya Israeli

1. “Pigeni baragumu!Adui anakuja kama taikuivamia nyumba ya Mwenyezi-Mungu,kwa kuwa wamelivunja agano languna kuiasi sheria yangu.

2. Waisraeli hunililia wakisema:‘Mungu wetu, sisi tunakujua.’

3. Lakini Israeli amepuuza mambo mema,kwa hiyo, sasa adui watamfuatia.

4. “Walijiwekea wafalme bila kibali changu,walijiteulia viongozi ambao sikuwatambua.Wamejitengenezea miungu ya fedha na dhahabu,jambo ambalo litawaangamiza.

5. Watu wa Samaria, naichukia sanamu yenu ya ndama.Hasira yangu inawaka dhidi yenu.Mtaendelea mpaka lini kuwa na hatia?

6. Nanyi Waisraeli ni hivyohivyo!Na sanamu yenu hiyo fundi ndiye aliyeitengeneza.Yenyewe si Mungu hata kidogo.Naam! Sanamu ya ndama ya Samaria itavunjwavunjwa!

7. “Wanapanda upepo, watavuna kimbunga!Mimea yao ya nafaka iliyo mashambanihaitatoa nafaka yoyote.Na hata kama ikizaa,mazao yake yataliwa na wageni.

8. Waisraeli wamemezwa;sasa wamo kati ya mataifa mengine,kama chombo kisicho na faida yoyote;

9. kwa kuwa wamekwenda kuomba msaada Ashuru.Efraimu ni punda anayetangatanga peke yake;Efraimu amekodisha wapenzi wake.

10. Wametafuta wapenzi kati ya watu wa mataifa,lakini mimi nitawakusanya mara.Na hapo watasikia uzito wa mzigo,ambao mfalme wa wakuu aliwatwika.

11. “Watu wa Efraimu wamejijengea madhabahu nyingi,na madhabahu hizo zimewazidishia dhambi.

12. Hata kama ningewaandikia sheria zangu mara nyingi,wao wangeziona kuwa kitu cha kigeni tu.

13. Wanapenda kutoa tambiko,na kula nyama yake;lakini mimi Mwenyezi-Mungu sipendezwi hata kidogo.Mimi nayakumbuka makosa yao;nitawaadhibu kwa dhambi zao;nitawarudisha utumwani Misri.

14. Waisraeli wamemsahau Muumba wao,wakajijengea majumba ya fahari;watu wa Yuda wamejiongezea miji ya ngome,lakini mimi nitaipelekea moto miji hiyo,na kuziteketeza ngome zao.”