Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13
  14. 14

Agano la Kale

Agano Jipya

Hosea 7 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kila nikitaka kuwarekebisha watu wangu,ninapotaka kuwaponya Waisraeli,uovu wa watu wa Efraimu hufunuliwa,matendo mabaya ya Samaria hujitokeza.Wao huongozwa na udanganyifu,kwenye nyumba wezi huvunjanje barabarani wanyang'anyi huvamia.

2. Hawafikiri hata kidogo kwamba miminayakumbuka maovu yao yote.Sasa maovu yao yamewabana.Yote waliyotenda yako mbele yangu.

Uhaini katika ikulu

3. “Wanamfurahisha mfalme kwa maovu yaowanawafurahisha wakuu kwa uhaini wao.

4. Wote ni wazinzi;wao ni kama tanuri iliyowashwa motoambao mwokaji hauchochei tangu akande ungampaka mkate utakapoumuka.

5. Kwenye sikukuu ya mfalme,waliwalewesha sana maofisa wake;naye mfalme akashirikiana na wahuni.

6. Kama tanuri iwakavyo,mioyo yao huwaka kwa hila;usiku kucha hasira yao hufuka moshi,ifikapo asubuhi, hulipuka kama miali ya moto.

7. Wote wamewaka hasira kama tanuri,na wanawaangamiza watawala wao.Wafalme wao wote wameanguka,wala hakuna anayeniomba msaada.

Israeli anategemea mataifa mengine

8. “Efraimu amechanganyika na watu wa mataifa.Anaonekana kama mkate ambao haukugeuzwa.

9. Wageni wamezinyonya nguvu zake,wala yeye mwenyewe hajui;mvi zimetapakaa kichwani mwake,lakini mwenyewe hana habari.

10. Kiburi cha Waisraeli chashuhudia dhidi yao,hawanirudii mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wao;wala hawanitafuti kwa matukio hayo yote.

11. Efraimu ni kama njiwa, mjinga asiye na akili;mara yuko Misri, mara Ashuru kuomba.

12. Watakapokwenda nitatandaza wavu wangu niwanase,nitawaangusha chini kama ndege wa angani;nitamwaadhibu kadiri ya ripoti ya maovu yao.

13. Ole wao kwa kuwa wameniacha!Maangamizi na yawapate, maana wameniasi.Nilitaka kuwakomboa,lakini wanazua uongo dhidi yangu.

14. “Wananililia, lakini si kwa moyo.Wanagaagaa na kujikatakata vitandani mwao,kusudi nisikilize dua zao za nafaka na divai;lakini wanabaki waasi dhidi yangu.

15. Mimi ndimi niliyeiimarisha mikono yao,lakini wanafikiria maovu dhidi yangu.

16. Wanaigeukia miungu batili,wako kama uta uliolegea.Viongozi wao watakufa kwa upanga,kwa sababu ya maneno yao ya kiburi.Kwa hiyo, watadharauliwa nchini Misri.