Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 8:9-22 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Wenye hekima wenu wataaibishwa;watafadhaishwa na kunaswa.Wamelikataa neno la Mwenyezi-Mungu;je, ni hekima gani hiyo waliyo nayo?

10. Kwa hiyo, wake zao nitawapa watu wengine,mashamba yao nitawapa wengine.Maana, tangu mdogo hadi mkubwa,kila mmoja ana tamaa ya faida haramu.Tangu manabii hadi makuhani,kila mmoja anatenda kwa udanganyifu.

11. Wameliponya jeraha la watu wangu juujuu,wakisema, ‘Kuna amani, kuna amani’,kumbe hakuna amani yoyote!

12. Je, waliona aibu walipotenda machukizo hayo?La hasha! Hawakuona aibu hata kidogo.Hata hawajui kuona haya.Kwa hiyo, wataanguka pamoja na wale walioanguka;nitakapowaadhibu, wataangamia.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

13. “Mimi Mwenyezi-Mungu nasema:Nilipotaka kukusanya chochote kutoka kwao,sikupata zabibu hata moja juu ya mzabibu,sikupata tini zozote juu ya mtini;hata majani yao yamekauka.Hata nilichokuwa nimewapa kimetoweka.”

14. “Watu wanauliza: Kwa nini sisi tunakaa tu hapa?Kusanyikeni, tuingie katika miji yenye ngome,tukaangamie huko!Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, ametupangia tuangamie,ametupa maji yenye sumu tunywe,kwa kuwa tumemkosea yeye.

15. Tulitazamia kupata amani,lakini hakuna jema lililotokea.Tulitazamia wakati wa kuponywa,badala yake tukapata vitisho.

16. Sauti za farasi wao zinasikika,kwa mlio wa farasi wao wa vita,nchi nzima inatetemeka.Wanafika na kuiharibu nchi na vyote vilivyomo,kuangamiza mji pamoja na wote waishio humo.

17. “Basi nitawaleteeni nyoka;nyoka wenye sumu wasioweza kurogwa na walozi,nao watawauma nyinyi.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”

18. Huzuni yangu haiwezi kutulizwa,moyo wangu wasononeka ndani yangu.

19. Sikiliza kilio cha watu wangu,kutoka kila upande katika nchi.“Je, Mwenyezi-Mungu hayuko Siyoni?Je, mfalme wake hayuko tena huko?”“Mbona wamenikasirisha kwa sanamu zao za miungu,na vinyago vyao vya miungu ya kigeni?”

20. “Mavuno yamepita, kiangazi kimekwisha,nasi bado hatujaokolewa!

21. Jeraha la watu wangu limeniumiza moyoni,ninaomboleza na kufadhaika.

22. Je, hakuna dawa ya kupaka huko Gileadi?Je, hakuna mganga huko?Mbona basi watu wangu hawajaponywa?

Kusoma sura kamili Yeremia 8