Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 8:13-16 Biblia Habari Njema (BHN)

13. “Mimi Mwenyezi-Mungu nasema:Nilipotaka kukusanya chochote kutoka kwao,sikupata zabibu hata moja juu ya mzabibu,sikupata tini zozote juu ya mtini;hata majani yao yamekauka.Hata nilichokuwa nimewapa kimetoweka.”

14. “Watu wanauliza: Kwa nini sisi tunakaa tu hapa?Kusanyikeni, tuingie katika miji yenye ngome,tukaangamie huko!Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, ametupangia tuangamie,ametupa maji yenye sumu tunywe,kwa kuwa tumemkosea yeye.

15. Tulitazamia kupata amani,lakini hakuna jema lililotokea.Tulitazamia wakati wa kuponywa,badala yake tukapata vitisho.

16. Sauti za farasi wao zinasikika,kwa mlio wa farasi wao wa vita,nchi nzima inatetemeka.Wanafika na kuiharibu nchi na vyote vilivyomo,kuangamiza mji pamoja na wote waishio humo.

Kusoma sura kamili Yeremia 8