Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13

Agano la Kale

Agano Jipya

Nehemia 7 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Baada ya ukuta kukamilika, malango yote kuwa tayari, na kuteuliwa kwa walinzi, waimbaji na Walawi,

2. nilimteua ndugu yangu Hanani kuwa mwangalizi wa Yerusalemu akishirikiana na Hanania aliyekuwa mkuu wa ngome katika Yerusalemu; kwa sababu alikuwa mtu wa kutegemewa na anayemcha sana Mungu, hapakuwapo mwingine aliyelingana naye,

3. nikawaagiza, “Malango yasifunguliwe usiku kucha hadi jua linapokuwa limepanda. Kabla hawajaondoka walinzi ni lazima kufunga milango yote kwa makomeo yake. Teueni walinzi miongoni mwa wakazi wa mji wa Yerusalemu, kila mmoja awe mahali pake kukabiliana na nyumba yake.”

Orodha ya waliorudi kutoka uhamishoni

4. Mji wa Yerusalemu ulikuwa mpana na mkubwa, lakini wakazi wake walikuwa wachache na nyumba zilikuwa hazijajengwa.

5. Mungu akanipa moyo kuwakusanya viongozi na watu ili kujua koo zao. Nikapata kitabu cha koo za watu waliorudi toka uhamishoni mara ya kwanza, na hawa wafuatao ndio waliokuwa wameorodheshwa ndani yake.

6. Wale waliokuwa uhamishoni kule Babuloni, walirudi mjini Yerusalemu na nchini Yuda, kila mmoja akarudi mjini kwake. Jamaa zao walikuwa wamekaa Babuloni tangu mfalme Nebukadneza alipowahamishia huko wakiwa mateka.

7. Waliporudi waliongozwa na Zerubabeli, Yeshua, Nehemia, Azaria, Raamia, Nahamani, Mordekai, Bilshani, Misperethi, Bigwai, Nehumu na Baana. Ifuatayo ni idadi ya watu wa koo za Israeli waliorudi toka uhamishoni:

8. Watu wa ukoo wa Paroshi: 2,172;

9. wa ukoo wa Shefatia: 372;

10. wa ukoo wa Ara: 652;

11. wa ukoo wa Pahath-moabu, yaani wazawa wa Yeshua na Yoabu: 2,818;

12. wa ukoo wa Elamu: 1,254;

13. wa ukoo wa Zatu: 845;

14. wa ukoo wa Zakai: 760;

15. wa ukoo wa Binui: 648;

16. wa ukoo wa Bebai: 624;

17. wa ukoo wa Azgadi: 2,322;

18. wa ukoo wa Adonikamu: 667;

19. wa ukoo wa Bigwai: 2,067;

20. wa ukoo wa Adini: 655;

21. wa ukoo wa Ateri (ambao pia unaitwa Hezekia): 98;

22. wa ukoo wa Hashumu: 328;

23. wa ukoo wa Bezai: 324;

24. wa ukoo wa Harifu: 112;

25. wa ukoo wa Gibeoni: 95;

26. Watu wa miji ifuatayo pia walirudi: Wa mji wa Bethlehemu na Netofa: 188;

27. wa mji wa Anathothi: 128;

28. wa mji wa Beth-azmawethi: 42;

29. wa miji ya Kiriath-yearimu, Kefira na Beerothi: 743;

30. wa miji ya Rama na Geba: 621;

31. wa mji wa Mikmashi: 122;

32. wa miji ya Betheli na Ai: 123;

33. wa mji mwingine wa Nebo: 52;

34. wa mji mwingine wa Elamu: 1,254;

35. wa mji wa Harimu: 320;

36. wa mji wa Yeriko: 345;

37. wa miji ya Lodi, Hadidi na Ono: 721;

38. wa mji wa Senaa: 3,930.

39. Ifuatayo ni idadi ya makuhani waliorudi kutoka uhamishoni: Makuhani wa ukoo wa Yedaya, waliokuwa wazawa wa Yeshua: 973;

40. wa ukoo wa Imeri: 1,052;

41. wa ukoo wa Pashuri: 1247;

42. wa ukoo wa Harimu: 1017.

43. Walawi wa ukoo wa Yeshua, yaani Kadmieli, wazawa wa Hodavia waliorudi kutoka uhamishoni walikuwa 74.

44. Waimbaji: Wazawa wa Asafu walikuwa 148.

45. Walinzi: Wazawa wa Shalumu, wa Ateri, wa Talmoni, wa Akubu, wa Hatita na wa Shobai, walikuwa 138.

46. Koo za wahudumu hekaluni waliorudi kutoka uhamishoni zilikuwa: Ukoo wa Ziha, wa Hasufa, wa Tabaothi;

47. wa Kerosi, wa Siaha, wa Padoni;

48. wa Lebana, wa Hagaba, wa Shalmai;

49. wa Hanani, wa Gideli, wa Gahari;

50. wa Reaya, wa Resini, wa Nekoda;

51. wa Gazamu, wa Uza, wa Pasea;

52. wa Besai, wa Meunimu, wa Nefushesimu;

53. wa Bakbuki, wa Hakufa, wa Harhuri;

54. wa Baslithi, wa Mehida, wa Harsha;

55. wa Barkosi, wa Sisera, wa Tema;

56. wa Nezia na ukoo wa Hatifa.

57. Koo za wazawa wa watumishi wa mfalme Solomoni waliorudi kutoka uhamishoni zilikuwa: Ukoo wa Sotai, wa Soferethi, wa Perida;

58. wa Yaala, wa Darkoni, wa Gideli;

59. ukoo wa Shefatia, wa Hatili, wa Pokereth-hasebaimu na ukoo wa Amoni.

60. Basi wahudumu wote wa hekalu na wazawa wa watumishi wa Solomoni, waliorudi kutoka uhamishoni, walikuwa 392.

61. Watu wa miji ifuatayo, nao walirudi: Wa Tel-mela, wa Tel-harsha, wa Kerubu, wa Adoni na wa Imeri; ila haikuwezekana kuthibitisha kama walikuwa wazawa wa Waisraeli

62. wazawa wa Delaya, Tobia na wa Nekoda; jumla: Watu 642.

63. Wazawa wa koo zifuatazo za makuhani pia walirudi: Ukoo wa Hobaya, wa Hakozi na wa Barzilai (aliyekuwa ameoa binti za Barzilai, Mgileadi, naye akachukua jina la ukoo huo).

64. Hao walitafuta orodha yao kati ya wengine walioorodheshwa katika kumbukumbu za koo, lakini ukoo wao haukuwemo. Kwa hiyo hawakuruhusiwa kutiwa katika huduma ya ukuhani kwani walihesabiwa kuwa najisi.

65. Mtawala akawaambia kuwa hawaruhusiwi kushiriki chakula kitakatifu sana, mpaka afike kuhani mwenye kauli ya Urimu na Thumimu.

66. Watu wote waliorudi kutoka uhamishoni jumla yao ilikuwa 42,360.

67. Tena kulikuwa na watumishi wanaume na wanawake 7,337, nao walikuwa waimbaji wanaume na wanawake, wote 245.

68. Walikuwa na farasi 736, nyumbu 245,

69. ngamia 435, na punda 6,720.

70. Baadhi ya wakuu wa koo walichangia kazi ya ujenzi. Mtawala wa mkoa alitoa kilo 8 za dhahabu, mabirika 50, mavazi 530.

71. Baadhi ya wakuu wa koo walitoa kilo 168 za dhahabu, na kilo 1,250 za fedha.

72. Matoleo ya watu wengine wote yalikuwa kilo 168 za dhahabu, kilo 140 za fedha na mavazi ya makuhani 67.

73. Basi, makuhani, Walawi, walinzi wa hekalu, waimbaji, baadhi ya watu wengine, watumishi wa hekalu na watu wote wa Israeli, wakaishi katika miji yao.