Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9
  10. 10
  11. 11
  12. 12
  13. 13

Agano la Kale

Agano Jipya

Nehemia 9 Biblia Habari Njema (BHN)

Watu wanaungama dhambi zao

1. Siku ya ishirini na nne ya mwezi huo wa saba, watu wa Israeli walikusanyika, wakifunga na kuvaa mavazi ya magunia na kujipaka udongo kichwani kuonesha majuto yao.

2. Wakati huo, walikuwa wamejitenga mbali na watu wa mataifa mengine, wakasimama na kuungama dhambi zao na maovu ya babu zao.

3. Kwa muda wa kama masaa matatu, walisimama huku sheria ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wao, inasomwa. Na kwa masaa matatu yaliyofuata, walikuwa wakitubu na kumwabudu Mwenyezi-Mungu, Mungu wao.

4. Kuliwekwa jukwaa la Walawi; hapo walisimama Yeshua, Bani, Kadmieli, Shebania, Buni, Sherebia, Bani na Kenani. Wakamwomba kwa sauti kubwa Mwenyezi-Mungu, Mungu wao.

5. Walawi, yaani: Yeshua, Kadmieli, Bani, Hashabuea, Sherebia, Hodia, Shebania na Pethahia wakawaambia watu;“Simameni na kumsifu Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu.Msifuni milele na milele!Na watu walisifu jina lako tukufu,ambalo hutukuka kuliko baraka na sifa zote.”

Sala ya toba

6. Ezra akaomba kwa sala ifuatayo:“Wewe peke yako ndiwe Mwenyezi-Mungu;ndiwe uliyefanya mbingu na jeshi lake lote,dunia na vyote vilivyomo,bahari na vyote vilivyomo;nawe ndiwe unayevihifadhi hai,na jeshi lote la mbinguni lakuabudu wewe.

7. Wewe ndiwe Mwenyezi-Mungu,Mungu uliyemchagua Abramu,ukamtoa toka Uri ya Wakaldayona kumpa jina Abrahamu.

8. Ukamwona kuwa yu mwadilifu mbele yako;ukafanya agano naye kuwapa wazawa wake nchi ya Wakanaani,Wahiti, Waamori, Waperizi, Wayebusi na Wagirgashi.Na ahadi yako ukaitimiza;kwani wewe u mwaminifu.

9. “Uliyaona mateso ya babu zetuwalipokuwa nchini Misri,na walipokuomba msaada kwenye Bahari ya Shamuuliwasikia.

10. Ulifanya ishara na maajabu dhidi ya Farao,watumishi wake wotena watu wote wa nchi yake;kwani ulijua kuwawaliwakandamiza babu zetu.Ukajipatia umaarufu uliopo mpaka leo.

11. Uliigawa bahari katikati mbele yao,nao wakapita katikati ya bahari,mahali pakavu.Lakini ukawatupa Wamisri waliowafuatiakama jiwe zito ndani ya maji mengi.

12. Mchana uliwaongoza kwa mnara wa wingu,na usiku uliwaongoza kwa mnara wa motoili kuwamulikia njia ya kuendea.

13. Kule mlimani Sinaiulishuka toka mbinguni na kuzungumza nao.Ukawapa maagizo safi, sheria za kweli,kanuni nzuri na amri.

14. Kwa njia ya Mose, mtumishi wako,ukawajulisha Sabato yako takatifuna ukawaagiza kuzifuata amri,kanuni na sheria ulizowaamrisha.

15. Walipokuwa na njaa,ukawapa chakula kutoka mbinguni.Walipokuwa na kiuukawapa maji kutoka kwenye mwamba.Ukawaagiza kuichukua nchi uliyokuwa umewaahidi.

16. Lakini wao na babu zetu wakawa na kiburina wakawa na shingo ngumuwakakataa kufuata maagizo yako.

17. Wakakataa kutii;wasiyakumbuke maajabu uliyofanya miongoni mwao.Wakawa na shingo zao ngumu,wakajichagulia kiongozi wa kuwarudishautumwani nchini Misri.Bali wewe Mungu u mwepesi kusamehe,mwenye neema na huruma,wewe hukasiriki upesi.U mwenye fadhili nyingi, na hukuwatupa.

18. Hata walipojitengenezea sanamu ya ndama na kusema,‘Huyu ndiye mungu wetualiyetutoa kutoka nchi ya Misri,’wakawa wamefanya kufuru kubwa.

19. Wewe kwa huruma zako nyingihukuwatupa kule jangwani.Mnara wa winguuliowaongoza mchana haukuondoka,wala mnara wa motouliowamulikia njia usiku, haukuondoka.

20. Ukawapa roho yako njema kuwashauri;ukawapa mana kuwa chakula chao na maji ya kunywaili kutuliza kiu chao.

21. Ukawatunza jangwani kwa miaka arubainina hawakukosa chochote;mavazi yao hayakuchakaawala nyayo zao hazikuvimba.

22. “Ukawaruhusu kushinda falme na mataifa,ukawafanyia mengi kila upande.Wakaishinda nchi ya Heshbonialikotawala mfalme Sihoni;na tena wakaishinda nchi ya Bashanialikotawala mfalme Ogu.

23. Wazawa wao ukawafanya wawe wengikama nyota za mbinguni;ukawaleta katika nchiuliyowaahidi babu zao.

24. Hivyo, hao wazawa wakaja na kuimiliki nchi;uliwashinda wakazi wa nchi hiyo,Wakanaani, ukawatia mikononi mwao,pamoja na wafalme wao,watu wao na nchi yao ili wawatende wapendavyo.

25. Miji yenye ngome wakaiteka,wakachukua nchi yenye utajiri,majumba yenye vitu vingi vizuri,visima vilivyochimbwa,mashamba ya mizabibu na mizeitunipamoja na miti yenye matunda kwa wingi.Hivyo wakala,wakashiba na kunenepana kuufurahia wema wako.

26. Lakini hawakuwa waaminifu kwako.Wakakuasi,wakaiacha sheria yakona kuwaua manabii waliowaonyaili wakurudie wewe.Wakakufuru sana.

27. Hivyo, ukawatia katika mikono ya adui zao,nao wakawatesa.Lakini wakiwa katika mateso yao,wakakulilia, nawe ukawasikia kutoka mbinguni.Na kwa huruma zako nyingi,ukawapelekea viongozi wa kuwaokoa;nao wakawakomboa toka mikononi mwao.

28. Lakini amani ilipopatikanawakatenda dhambi tena mbele yako,nawe ukawaacha watiwe katikamikono ya adui zao wawatawale.Hata hivyo, walipotubu na kukuliliaukawasikiliza kutoka mbinguni.Na kwa kulingana na huruma zako nyingi,ukawaokoa mara nyingi.

29. Ukawaonya ili wairudie sheria yako.Hata hivyo, kwa kiburi chao,wakaacha kuzitii amri zako.Wakayaasi maagizo yako,ambayo kwayo mtu akiyatii, ataishi.Wakawa wajeuripia wakafanya shingo zao ngumu,na wakakataa kuwa watiifu.

30. Ukawavumilia kwa miaka mingi,na kuwaonya kwa njia ya roho yakokwa kupitia manabii wako;hata hivyo hawakusikiliza.Basi ukawaachaukawatia mikononi mwa mataifa mengine.

31. Hata hivyo,kutokana na huruma zako nyingi,hukuwaacha waangamie kabisa au kuwatupa,kwani wewe u Mungu mwenye neemana huruma.

32. Kwa hiyo, ee Mungu wetu,Mungu Mkuu,mwenye nguvu na wa kutisha,wewe unalishika agano lakona una fadhili nyingi.Mateso yaliyotupata, sisi,wafalme wetu, wakuu wetu,makuhani wetu, manabii wetu,babu zetu na watu wako wotetangu wakati wa wafalme wa Ashuru mpaka leo,usiyaone kuwa ni madogo.

33. Hata hivyo,unayo haki kwa kutuadhibu hivyo;kwani wewe umekuwa mwaminifuambapo sisi tumekuwa watenda maovu.

34. Wafalme wetu, wakuu wetu,makuhani wetu na babu zetuhawajaishika sheria yakowala kujali amri yakona maonyo yako uliyowapa.

35. Hawakukutumikia katika ufalme wao,wala walipoyafurahia mema yako mengi uliyowajalia kwa wingi,katika nchi kubwa na yenye rutuba uliyowapahawakuyaacha matendo yao maovu.

36. Na leo tumekuwa watumwa;tu watumwa katika nchi uliyowapa babu zetuwafurahie matunda na vipawa vyake vyema.

37. Kwa sababu ya dhambi zetu,utajiri wa nchi hiiunawaendea wafalme uliowaleta kututawala.Wanatutawala wapendavyohata na mifugo yetuwanaitendea wapendavyo,tumo katika dhiki kuu.”

Watu wanatia sahihi mapatano

38. Kutokana na haya yote yaliyotokea, sisi tunaweka agano imara na wakuu wetu kwa maandishi; Walawi na makuhani wanatia sahihi zao na mhuri wao.