Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7

Agano la Kale

Agano Jipya

Mika 1 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Neno la Mwenyezi-Mungu lilimjia Mika, mwenyeji wa Moreshethi, wakati Yothamu, Ahazi na Hezekia walipokuwa wafalme wa Yuda. Mika aliona mambo yote haya kuhusu Samaria na Yerusalemu.

Mwenyezi-Mungu aja kuhukumu

2. Sikilizeni enyi watu wote;sikiliza ewe dunia na vyote vilivyomo.Mwenyezi-Mungu anakuja kuwashtaki,Bwana anena kutoka hekalu lake takatifu.

3. Naam! Mwenyezi-Mungu yuaja kutoka makao yake;atashuka na kutembea juu ya vilele vya dunia.

4. Milima itayeyuka chini ya nyayo zake,kama nta karibu na moto;mabonde yatapasuka,kama maji yaporomokayo kwenye mteremko.

5. Haya yote yatatukiakwa sababu ya makosa ya wazawa wa Yakobo,kwa sababu ya dhambi za wazawa wa Israeli.Je, uhalifu wa Yakobo waonekana wapi?Katika mji wake mkuu Samaria!Je, uhalifu wa Yuda waonekana wapi?Katika Yerusalemu kwenyewe!

6. Kwa hiyo, Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Mji wa Samaria nitaufanya magofu nyikani,shamba ambalo watu watapanda mizabibu.Mawe yaliyoujenga nitayatupa bondeni,na misingi yake nitaichimbuachimbua.

7. Sanamu zake zote zitavunjwavunjwa,kila kilichochumwa kitateketezwa kwa moto.Vinyago vyake vyote nitaviharibu.Vilirundikwa kutokana na ujira wa malaya,navyo vitatumiwa tena kulipia umalaya.”

Nabii anaomboleza juu ya Yerusalemu na Yuda

8. Kwa sababu hiyo, mimi nitalia na kuomboleza;nitatembea uchi na bila viatu.Nitaomboleza na kulia kama mbweha,nitasikitika na kulia kama mbuni.

9. Majeraha ya Samaria hayaponyeki,nayo yameipata pia Yuda;yamefikia lango la Yerusalemu,mahali wanapokaa watu wangu.

10. Msiitangaze habari hii huko Gathi,wala msilie machozi!Huko Beth-leafra mgaegae mavumbini kwa huzuni.

11. Nendeni enyi wakazi wa Shafiri,mkiwa uchi na wenye haya.Wakazi wa Zaanani msitoke nje ya mji wenu.Watu wa Beth-ezeli wanalia;msaada wao kwenu umeondolewa.

12. Wakazi wa Marothi wanangojea msaada kwa hamu kubwa,lakini maangamizi yaja kutoka kwa Mwenyezi-Mungukaribu kabisa na lango la Yerusalemu.

13. Enyi wakazi wa Lakishi,fungeni farasi wepesi na magari ya vita.Nyinyi mlikuwa mmeiga dhambi ya watu wa Siyoni,makosa ya Waisraeli yalikuwa kwenu.

14. Hivyo, mnapaswa kuagana na kuwaacha wakazi wa Morasheth-gathi.Nao mji wa Akzibu hautawasaidia wafalme wa Israeli,

15. Enyi wakazi wa Maresha,Mungu atawaleteeni tena adui atakayewateka.Viongozi waheshimiwa wa Israeliwatakimbilia pangoni huko Adulamu.

16. Enyi watu wa Yuda, nyoeni uparakuwaombolezea watoto wenu wapenzi;panueni upara wenu uwe mpana kama wa tai,maana watoto wenu watawaacha kwenda uhamishoni.