Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7

Agano la Kale

Agano Jipya

Mika 5 Biblia Habari Njema (BHN)

Kiongozi mpya kutoka Bethlehemu

1. Jumuikeni mkajikusanye enyi watu wa Yerusalemu;mkisema: “Tumezingirwa, tumesongwa;naye kiongozi wa Israeli wanampiga shavuni kwa fimbo.”

2. Mwenyezi-Mungu asema,“Lakini wewe Bethlehemu katika Efratha,wewe ni mdogo tu kati ya jamii za Yuda,lakini kwako kutatoka mtawalaatakayetawala juu ya Israeli kwa niaba yangu.Asili yake ni ya zama za kale.”

3. Hivyo Mungu atawaacha watu wake kwa maadui,mpaka yule mama mjamzito atakapojifungua.Kisha ndugu zake waliobakia,watarudi na kuungana na Waisraeli wenzao.

4. Huyo mtawala atawachunga watu wake kwa nguvu ya Mwenyezi-Mungu,kwa fahari yake Mwenyezi-Mungu, Mungu wake.Watu wake wataishi kwa usalama,maana atakuwa mkuu mpaka miisho ya dunia.

5. Yeye ndiye atakayeleta amani.Waashuru wakivamia nchi yetu,na kuupenya ulinzi wetu,tutapeleka walinzi wawakabili,naam, tutawapeleka viongozi wetu kwa wingi.

Ukombozi na adhabu

6. Kwa silaha zao wataitawala nchi ya Ashuru,na kuimiliki nchi ya Nimrodi.Watatuokoa mikononi mwa Waashuru,watakapowasili mipakani mwa nchi yetuna kuanza kuivamia nchi yetu.

7. Wazawa wa Yakobo watakaobaki haiwameenea miongoni mwa mataifa mengi,watakuwa kama umande wa Mwenyezi-Mungu uburudishao,kama manyunyu yaangukayo penye nyasiambayo hayasababishwi na mtuwala kumtegemea binadamu.

8. Wazawa wa Yakobo watakaobaki hai,wameenea miongoni mwa mataifa na watu wengiwatakuwa na nguvu kubwakama simba kati ya wanyama wa porini,kama mwanasimba miongoni mwa makundi ya kondoo,ambaye kila mahali apitapo,huyarukia na kuyararua mawindo yake,asiwepo mtu yeyote wa kuyaokoa.

9. Waisraeli watawashinda adui zaona kuwaangamiza kabisa.

10. Mwenyezi-Mungu asema,“Wakati huo nitawaondoa farasi wenu,na kuyaharibu magari yenu ya farasi.

11. Nitaiharibu miji ya nchi yenu,na kuzibomolea mbali ngome zenu.

12. Nitatokomeza matendo yenu ya uchawi,nanyi hamtakuwa tena na wapiga ramli.

13. Nitaziharibu sanamu zenu,na nguzo zenu za ibada;nanyi mtakoma kuabudu vitu mlivyotengeneza wenyewe.

14. Nitazing'oa sanamu za Ashera kutoka kwenu,na kuiangamiza miji yenu.

15. Kwa hasira na ghadhabu yangu,nitalipiza kisasi mataifa yote yasiyonitii.”