Agano la Kale

Agano Jipya

Yoshua 18:17-26 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Huko, mpaka uligeuka kwenda kaskazini kuelekea En-shemeshi, ukapitia Gelilothi unaokabili mwinuko wa Adumimu na kuteremka hadi kwenye jiwe la Bohani mwana wa Reubeni.

18. Kutoka hapo, mpaka ulizunguka kaskazini kwenye ukingo wa juu wa Araba na kuishia huko Araba.

19. Tena, ukaendelea kwa upande wa kaskazini wa kilima cha Beth-hogla na kuishia kaskazini kabisa ya ghuba ya Bahari ya Chumvi, mahali unapoingilia mto Yordani. Huu ni mpaka wake kwa upande wa kusini.

20. Mto Yordani ndio uliokuwa mpaka wake upande wa mashariki. Ndivyo zilivyowekewa mipaka nchi zilizopewa koo za kabila la Benyamini.

21. Miji ya koo za kabila la Benyamini ni Yeriko, Beth-hogla, Emek-kesisi,

22. Beth-araba, Zemaraimu, Betheli,

23. Avimu, Para, Ofra,

24. Kefar-amoni, Ofni na Geba. Jumla ya miji waliyopewa ni kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.

25. Miji mingine ni Gibeoni, Rama, Beerothi,

26. Mizpa, Kefira, Moza,

Kusoma sura kamili Yoshua 18