Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 6:4-16 Biblia Habari Njema (BHN)

4. Watasema: “Jitayarisheni kuushambulia Siyoni.Haya! Tuanze kushambulia adhuhuri!Bahati mbaya; jua linatua!Kivuli cha jioni kinarefuka.

5. Basi, tutaushambulia usiku;tutayaharibu majumba yake ya kifalme.”

6. Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema:“Kateni miti yake,rundikeni udongo kuuzingira Yerusalemu.Mji huu ni lazima uadhibiwe,maana hamna lolote ndani yake ila dhuluma.

7. Kama kisima kinavyohifadhi maji yake yakabaki safi,ndivyo Yerusalemu unavyohifadhi uovu wako.Ukatili na uharibifu vyasikika ndani yake,magonjwa na majeraha yake nayaona daima.

8. Hilo na liwe onyo kwako ee Yerusalemu,la sivyo nitakutupa kabisa kwa chuki;nikakufanya uwe jangwa,mahali pasipokaliwa na mtu.”

9. Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema hivi:“Kusanyeni watu wote wa Israeli waliobakikama watu wakusanyavyo zabibu zote;kama afanyavyo mchumazabibu,pitisheni tena mikono yenu katika matawi yake.”

10. Nitaongea na nani nipate kumwonya,ili wapate kunisikia?Tazama, masikio yao yameziba,hawawezi kusikia ujumbe wako.Kwao neno lako, ee Mwenyezi-Mungu,limekuwa jambo la dhihaka,hawalifurahii hata kidogo.

11. Nimejaa hasira ya Mwenyezi-Mungu dhidi yao.Nashindwa kuizuia ndani yangu.Mwenyezi-Mungu akaniambia:“Imwage hasira barabarani juu ya watotona pia juu ya makundi ya vijana;wote, mume na mke watachukuliwa,kadhalika na wazee na wakongwe.

12. Nyumba zao zitapewa watu wengine,kadhalika na mashamba yao na wake zao;maana nitaunyosha mkono wangu,kuwaadhibu wakazi wa nchi hii.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

13. Wote, tangu mdogo hadi mkubwa kabisa,kila mmoja anatamani kupata faida isiyo halali.Tangu manabii hadi makuhani,kila mmoja wao ni mdanganyifu.

14. Wameliponya jeraha la watu wangu juujuu,wanasema; ‘Amani, amani’,kumbe hakuna amani yoyote!

15. Je, waliona aibu walipofanya machukizo hayo?La! Hawakuona aibu hata kidogo.Hawakujua hata namna ya kuona aibu.Kwa hiyo wataanguka pamoja na wale waangukao;wakati nitakapowaadhibu,wataangamizwa kabisa.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”

16. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Simameni katika njia panda, mtazame.Ulizeni mjue juu ya matukio ya zamani.Tafuteni mahali ilipo njia nzurimuifuate nanyi mtapumzisha nafsi zenu.Lakini wao wakasema:‘Hatutafuata njia hiyo.’

Kusoma sura kamili Yeremia 6