Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 6:22-25 Biblia Habari Njema (BHN)

22. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Tazameni, watu wanakuja toka nchi ya kaskazini;taifa kubwa linajitayarisha kutoka mbali duniani.

23. Wamezishika pinde zao na mikuki,watu wakatili wasio na huruma.Vishindo vyao ni kama ngurumo ya bahari.Wamepanda farasi,wamejipanga tayari kwa vita,dhidi yako ewe Siyoni!”

24. Waisraeli wanasema,“Tumesikia habari zao,mikono yetu imelegea;tumeshikwa na dhiki na uchungu,kama mwanamke anayejifungua.

25. Hatuwezi kwenda mashambani,wala kutembea barabarani;maadui wameshika silaha mikononi,vitisho vimejaa kila mahali.”

Kusoma sura kamili Yeremia 6