Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 6:20-29 Biblia Habari Njema (BHN)

20. Ya nini kuniletea ubani kutoka Sheba,na udi wa harufu nzuri kutoka nchi ya mbali?Sadaka zenu za kuteketezwa hazikubaliki,wala tambiko zenu hazinipendezi.

21. Kwa hiyo mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi:Tazama, nitawawekea watu hawa vikwazoambavyo vitawakwaza na kuwaangusha chini.Akina baba na watoto wao wa kiume wataangamia,kadhalika na majirani na marafiki.”

22. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Tazameni, watu wanakuja toka nchi ya kaskazini;taifa kubwa linajitayarisha kutoka mbali duniani.

23. Wamezishika pinde zao na mikuki,watu wakatili wasio na huruma.Vishindo vyao ni kama ngurumo ya bahari.Wamepanda farasi,wamejipanga tayari kwa vita,dhidi yako ewe Siyoni!”

24. Waisraeli wanasema,“Tumesikia habari zao,mikono yetu imelegea;tumeshikwa na dhiki na uchungu,kama mwanamke anayejifungua.

25. Hatuwezi kwenda mashambani,wala kutembea barabarani;maadui wameshika silaha mikononi,vitisho vimejaa kila mahali.”

26. Mwenyezi-Mungu asema,“Jivikeni mavazi ya gunia, enyi watu wanguna kugaagaa katika majivu.Ombolezeni kwa uchungu,kama mtu anayemwombolezea mwana wa pekee,maana mwangamizi atakuja,na kuwashambulia ghafla.

27. Yeremia, wewe nimekuweka kuwa mchunguzina mpimaji wa watu wangu,ili uchunguze na kuzijua njia zao.

28. Wote ni waasi wakaidi,ni watu wanaopitapita wakisengenya wengine,wagumu kama shaba nyeusi au chuma;wote hutenda kwa ufisadi.

29. Mifuo inafukuta kwa nguvu,risasi inayeyukia humohumo motoni;ni bure kuendelea kuwatakasa watu wangu,waovu hawawezi kuondolewa uchafu wao.

Kusoma sura kamili Yeremia 6