Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 5:15-27 Biblia Habari Njema (BHN)

15. “Nami Mwenyezi-Mungu nasema juu yenu enyi Waisraeli:Mimi naleta taifa moja kutoka mbali,lije kuwashambulia.Taifa ambalo halishindiki,taifa ambalo ni la zamani,ambalo lugha yake hamuifahamu,wala hamwezi kuelewa wasemacho.

16. Mishale yao husambaza kifo;wote ni mashujaa wa vita.

17. Watayala mazao yenu na chakula chenu;watawamaliza watoto wenu wa kike na wa kiume.Watachinja makundi yenu ya kondoo na ng'ombe;wataiharibu mizabibu yenu na mitini yenu.Miji yenu ya ngome mnayoitegemea,wataiharibu kwa silaha zao.

18. “Lakini, hata katika siku hizo mimi Mwenyezi-Mungu nasema, sitawaangamiza na kuwamaliza kabisa.

19. Na watu wenu watakapouliza ‘Kwa nini Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, ametutendea mambo hayo yote?’ Wewe utawaambia, ‘Nyinyi mlimwacha Mwenyezi-Mungu, mkaitumikia miungu ya kigeni katika nchi yenu. Basi ndivyo mtakavyowatumikia watu wengine katika nchi isiyo yenu.’

20. “Watangazie wazawa wa Yakobo,waambie watu wa Yuda hivi:

21. Sikilizeni enyi wajinga na wapumbavu;watu mlio na macho, lakini hamwoni,mlio na masikio, lakini hamsikii.

22. Mbona hamniogopi? Nauliza mimi Mwenyezi-Mungu!Kwa nini hamtetemeki mbele yangu?Mimi niliweka mchanga uwe mpaka wa bahari,kizuizi cha daima ambacho bahari haiwezi kuvuka.Ingawa mawimbi yanaupiga, hayawezi kuupita;ingawa yananguruma, hayawezi kuuruka.

23. Lakini watu hawa wana moyo wa ukaidi na uasi;wameniacha wakaenda zao.

24. Wala hawasemi mioyoni mwao;‘Na tumche Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu,anayetujalia mvua kwa wakati wake,anayetupatia mvua za masika na mvua za vuli;na kutupa majira maalumu ya mavuno.’

25. Makosa yenu yamewazuia msipate baraka hizo,dhambi zenu zimewafanya msipate mema.

26. Naam, kuna walaghai miongoni mwa watu wangu,watu ambao hunyakua mali za wengine.Wako kama wawindaji wa ndege:Hutega mitego yao na kuwanasa watu.

27. Kama vile kapu lililojaa ndege walionaswa,ndivyo nyumba zao zilivyojaa mali za udanganyifu.Ndiyo maana wamekuwa watu wakubwa na matajiri,

Kusoma sura kamili Yeremia 5