Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 46:13-26 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Neno ambalo Mwenyezi-Mungu alimwambia Yeremia wakati alipofika Nebukadneza mfalme wa Babuloni kuishambulia nchi ya Misri:

14. “Tangaza nchini Misri,piga mbiu huko Migdoli,tangaza huko Memfisi na Tahpanesi.Waambie: ‘Kaeni tayari kabisamaana upanga utawaangamiza kila mahali.’

15. Kwa nini shujaa wako amekimbia?Mbona fahali wako hakuweza kustahimili?Kwa sababu mimi Mwenyezi-Mungu nilimwangusha chini!

16. Wengi walijikwaa, wakaanguka,kisha wakaambiana wao kwa wao:‘Simameni, tuwaendee watu wetu,turudi katika nchi yetu,tuukimbie upanga wa adui.’

17. “Naye Farao, mfalme wa Misri, mpangeni jina hili:‘Kishindo kitupu!’

18. Mimi naapa kwa uhai wangunasema mimi mfalme niitwaye Mwenyezi-Mungu wa majeshi,kweli adui anakuja kuwashambulieni:Ni hakika kama Tabori ulivyo mlimakama mlima Karmeli uonekanavyo kutoka baharini.

19. Enyi wakazi wa Misrijitayarisheni na mizigo kwenda uhamishoni!Maana mji wa Memfisi utaharibiwa kabisa,utakuwa magofu yasiyokaliwa na watu.

20. Misri ni kama mtamba mzuri wa ng'ombe,lakini kipanga kutoka kaskazini amemvamia.

21. Hata askari wake wa kukodiwa ni kama ndama wanono;nao pia wamegeuka, wakakimbia pamoja,wala hawakuweza kustahimili,kwa maana siku yao ya kuangamizwa imefika,wakati wao wa kuadhibiwa umewadia.

22. Misri anatoa sauti kama nyoka anayekimbia;maana maadui zake wanamjia kwa nguvu,wanamjia kwa mashoka kama wakata-miti.

23. Wataukata kabisa msitu wake, ingawa haupenyeki,nasema mimi Mwenyezi-Mungu,maana wao ni wengi kuliko nzige wasiohesabika.

24. Watu wa Misri wataaibishwa,watatiwa mikononi mwa watu kutoka kaskazini.”

25. Mwenyezi-Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, alisema: “Tazama, mimi nitamwadhibu Amoni mungu wa Thebesi, nitaiadhibu Misri na miungu yake na wafalme wake, nitamwadhibu Farao na wote wanaomtegemea.

26. Nitawatia mikononi mwa wale wanaotaka kuyaangamiza maisha yao, yaani Nebukadneza mfalme wa Babuloni na maofisa wake. Baadaye, nchi ya Misri itakaliwa na watu kama ilivyokuwa hapo zamani. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

Kusoma sura kamili Yeremia 46