Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 4:1-11 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Ukitaka kurudi ee Israeli, nirudie mimi.Ukiviondoa vitu vya kuchukiza mbele yangu,usipotangatanga huko na huko,

2. ukiapa kwa ukweli, unyofu na uadilifu,kwa kusema, ‘Kama Mwenyezi-Mungu aishivyo’,ndipo mataifa yatakapopata baraka kwangu,na kutukuka kwa sababu yangu.”

3. Mwenyezi-Mungu awaambia hivi watu wa Yuda na wakazi wa Yerusalemu:“Limeni mashamba yenu mapya;msipande mbegu zenu penye miiba.

4. Enyi watu wa Yuda na wakazi wa Yerusalemu,jitakaseni kwa ajili yangu mimi Mwenyezi-Mungu,wekeni mioyo yenu wazi mbele yangu.La sivyo, ghadhabu yangu itachomoza kama moto,iwake hata pasiwe na mtu wa kuizima,kwa sababu ya uovu wa matendo yenu.

5. “Tangazeni huko Yuda,pazeni sauti huko Yerusalemu!Pigeni tarumbeta kila mahali nchini!Pazeni sauti na kusema:Kusanyikeni pamoja!Kimbilieni miji yenye ngome!

6. Twekeni bendera ya vita kuelekea Siyoni,kimbilieni usalama wenu, msisitesite!Mwenyezi-Mungu analeta maafana maangamizi makubwa kutoka kaskazini.

7. Kama simba atokavyo mafichoni mwake,mwangamizi wa mataifa ameanza kuja,anakuja kutoka mahali pake,ili kuiharibu nchi yako.Miji yako itakuwa magofu matupu,bila kukaliwa na mtu yeyote.

8. Kwa hiyo, vaa vazi la gunia,omboleza na kulia;maana, hasira kali ya Mwenyezi-Mungu,bado haijaondoka kwetu.

9. Mwenyezi-Mungu asema hivi: “Siku hiyo, mfalme na wakuu watakufa moyo; makuhani watapigwa na bumbuazi, na manabii watashangaa.”

10. Kisha nikasema: “Aa, Mwenyezi-Mungu, hakika umewadanganya kabisa watu hawa na mji wa Yerusalemu! Uliwaambia mambo yatawaendea vema, kumbe maisha yao yamo hatarini kabisa!”

11. Wakati huo, wataambiwa hivi watu hawa pamoja na mji wa Yerusalemu, “Upepo wa hari kutoka vilele vikavu vya jangwani utawavumia watu wangu. Huo si upepo wa kupepeta au kusafisha,

Kusoma sura kamili Yeremia 4