Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 31:1-12 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mwenyezi-Mungu asema: “Wakati utakuja ambapo nitakuwa Mungu wa jamaa zote za Israeli nao watakuwa watu wangu.

2. Mimi Mwenyezi-Mungu nasema:Watu walionusurika kuuawaniliwaneemesha jangwani.Wakati Israeli alipotafuta kupumzika,

3. mimi Mwenyezi-Mungu nilimtokea kwa mbali.Nami nimekupenda kwa mapendo ya daima,kwa hiyo nimeendelea kuwa mwaminifu kwako.

4. Nitakujenga upya nawe utajengeka,ewe Israeli uliye mzuri!Utazichukua tena ngoma zakoucheze kwa furaha na shangwe.

5. Utapanda tena mizabibujuu ya milima ya Samaria;wakulima watapanda mbeguna kuyafurahia mazao yake!

6. Maana siku yaja ambapo mlinzi atapiga mbiukatika vilima vya Efraimu:‘Amkeni, twende juu mpaka Siyonikwa Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu.’”

7. Maana Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Imbeni kwa furaha kwa ajili ya Yakobo,pigeni vigelegele kwa ajili ya taifa kuu,tangazeni, shangilieni na kusema:‘Mwenyezi-Mungu na awaokoe watu wake,amewaletea ukombozi waliobaki wa Israeli!’

8. Tazama, nitawaleta kutoka nchi ya kaskazini,nitawakusanya kutoka miisho ya dunia.Wote watakuwapo hapo;hata vipofu na vilema,wanawake waja wazito na wanaojifungua;umati mkubwa sana utarudi hapa.

9. Watarudi wakiwa wanatoa machozi,nitawarudisha nikiwafariji;nitawapitisha kando ya vijito vya maji,katika njia iliyonyoka ambamo hawatajikwaa;maana mimi nimekuwa baba wa Israeli,Efraimu ni mzaliwa wangu wa kwanza.

10. Enyi mataifa, sikilizeni neno langu mimi Mwenyezi-Mungu,litangazeni katika nchi za mbali,semeni: ‘Aliyemtawanya Israeli, atamkusanya,atamtunza kama mchungaji atunzavyo kondoo wake.’

11. Maana mimi Mwenyezi-Mungu nimemkomboa Yakobo,nimemwokoa kutoka kwa wenye nguvu kuliko yeye.

12. Watakuja na kuimba kwa sauti juu ya mlima Siyoni,wataona fahari juu ya wema wangu mimi Mwenyezi-Mungu,kwa nafaka, divai na mafuta niwapavyo,kwa kondoo na ng'ombe kadhalika;maisha yao yatakuwa kama bustani iliyotiliwa maji,wala hawatadhoofika tena.

Kusoma sura kamili Yeremia 31