Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 22:14-20 Biblia Habari Njema (BHN)

14. Wewe wasema:‘Nitalijenga jumba kubwa,lenye vyumba vikubwa ghorofani.’Kisha huifanyia madirisha,ukafunika kuta zake kwa mbao za mierezi,na kuipaka rangi nyekundu!

15. Unadhani umekuwa mfalmekwa kushindana kujenga kwa mierezi?Baba yako alikula na kunywa,akatenda mambo ya haki na memandipo mambo yake yakamwendea vema.

16. Aliwapatia haki maskini na wahitaji,na mambo yake yakamwendea vema.Hii ndiyo maana ya kunijua mimi Mwenyezi-Mungu.

17. Lakini macho yako wewe na moyo wako,hungangania tu mapato yasiyo halali.Unamwaga damu ya wasio na hatia,na kuwatendea watu dhuluma na ukatili.

18. “Kwa hiyo, mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi juu ya Yehoyakimu mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda:Wakati atakapokufa,hakuna atakayemwombolezea akisema,‘Ole, kaka yangu!’‘Ole, dada yangu!’Hakuna atakayemlilia akisema,‘Maskini, bwana wangu!’‘Maskini, mfalme wangu!’

19. Atazikwa bila heshima kama punda,ataburutwa na kutupiliwa mbali,nje ya malango ya Yerusalemu.”

20. Enyi watu wa Yerusalemu,pandeni Lebanoni mpige kelele,pazeni sauti zenu huko Bashani;lieni kutoka milima ya Abarimu,maana wapenzi wenu wote wameangamizwa.

Kusoma sura kamili Yeremia 22