Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 22:11-18 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Maana, Mwenyezi-Mungu asema hivi juu ya Shalumu mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, aliyetawala baada ya Yosia baba yake, na ambaye aliondoka mahali hapa: “Shalumu hatarudi tena mahali hapa,

12. bali atafia hukohuko walikomchukua utumwani. Kamwe hataiona tena nchi hii.

13. “Ole wako Yehoyakimuwewe unayejenga nyumba kwa dhulumana kuiwekea ghorofa bila kutumia haki.Unawaajiri watu wakutumikie burewala huwalipi mishahara yao.

14. Wewe wasema:‘Nitalijenga jumba kubwa,lenye vyumba vikubwa ghorofani.’Kisha huifanyia madirisha,ukafunika kuta zake kwa mbao za mierezi,na kuipaka rangi nyekundu!

15. Unadhani umekuwa mfalmekwa kushindana kujenga kwa mierezi?Baba yako alikula na kunywa,akatenda mambo ya haki na memandipo mambo yake yakamwendea vema.

16. Aliwapatia haki maskini na wahitaji,na mambo yake yakamwendea vema.Hii ndiyo maana ya kunijua mimi Mwenyezi-Mungu.

17. Lakini macho yako wewe na moyo wako,hungangania tu mapato yasiyo halali.Unamwaga damu ya wasio na hatia,na kuwatendea watu dhuluma na ukatili.

18. “Kwa hiyo, mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi juu ya Yehoyakimu mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda:Wakati atakapokufa,hakuna atakayemwombolezea akisema,‘Ole, kaka yangu!’‘Ole, dada yangu!’Hakuna atakayemlilia akisema,‘Maskini, bwana wangu!’‘Maskini, mfalme wangu!’

Kusoma sura kamili Yeremia 22