Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 17:8-23 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Huyo ni kama mti uliopandwa kando ya maji,upenyezao mizizi yake karibu na chemchemi.Hauogopi wakati wa joto ufikapo,majani yake hubaki mabichi.Hauhangaiki katika mwaka wa ukame,na hautaacha kuzaa matunda.

9. “Moyo wa mtu ni mdanganyifu kuliko vitu vyote;hauwezi kuponywa, hakuna awezaye kuuelewa!

10. Mimi Mwenyezi-Mungu hupima akilina kuchunguza mpaka ndani ya moyo wa mtu.Na hivyo humtendea kila mmoja,kulingana na mwenendo wake,kadiri ya matendo yake.”

11. Mtu apataye mali isiyo halalini kama kware akusanyaye makinda ambayo hakuyaangua:Wakati wa kilele cha ujana wake itamchopoka,na mwishoni atakuwa mtu mpumbavu.

12. Kuna kiti cha enzi kitukufukiti kilichoinuliwa juu;huko ndiko mahali petu patakatifu.

13. Ee Mwenyezi-Mungu tumaini la Israeli,wote wanaokukataa wataaibishwa;wanaokuacha wewe watatoweka,kama majina yaliyoandikwa vumbini,kwa maana wamekuacha wewe Mwenyezi-Mungu,uliye chemchemi ya maji ya uhai.

14. Uniponye, ee Mwenyezi-Mungu, nami nitapona;uniokoe, nami nitaokoka;maana, wewe ndiwe sifa yangu.

15. Tazama watu wanavyoniambia:“Jambo alilotishia Mwenyezi-Mungu liko wapi?Acha basi lije!”

16. Sikuikimbia huduma yako ya kuwa mchungajiwala sikutamani ile siku ya maafa ije.Wewe mwenyewe wajua nilichosema kwa mdomo wangu,nilichotamka wakijua waziwazi.

17. Usiwe tisho kwangu;wewe ndiwe kimbilio langu siku ya maafa.

18. Waaibishwe wale wanaonitesa,lakini mimi usiniache niaibike.Wafedheheshwe watu hao,lakini mimi usiniache nifedheheke.Uwaletee siku ya maafa,waangamize kwa maangamizi maradufu!

19. Mwenyezi-Mungu aliniambia hivi: “Nenda ukasimame penye lango la watu ambapo wafalme wa Yuda huingia na kutoka mjini, na katika malango mengine yote ya Yerusalemu useme:

20. Sikieni neno la Mwenyezi-Mungu enyi wafalme wa Yuda, nanyi watu wa Yuda na wakazi wa Yerusalemu ambao huingia kwa kupitia malango haya.

21. Waambie kwamba mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Kwa usalama wa maisha yenu, muwe na hadhari msije mkabeba mzigo siku ya Sabato, au kuingiza mzigo mjini kupitia malango ya Yerusalemu.

22. Msibebe mzigo kutoka majumbani mwenu siku ya Sabato wala kufanya kazi. Iadhimisheni siku ya Sabato kama siku takatifu kama nilivyowaamuru wazee wenu.

23. Lakini wazee wenu hawakunisikiliza wala kujali, bali walivifanya vichwa vyao kuwa vigumu, wakakataa kusikia na kufuata maagizo yangu.

Kusoma sura kamili Yeremia 17