Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 13:8-23 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Ndipo neno la Mwenyezi-Mungu likanijia:

9. “Mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Hivi ndivyo nitakavyokiharibu kiburi cha Yuda na kiburi kikubwa cha Yerusalemu.

10. Watu hawa waovu wanakataa kusikia maneno yangu, na badala yake wanakuwa wakaidi na kufuata mawazo yao wenyewe. Wanaifuata miungu mingine, wanaitumikia na kuiabudu. Hao watakuwa kama kikoi hiki ambacho hakifai kitu.

11. Kama vile kikoi kinavyoshikamana na kiuno cha mtu, ndivyo nilivyowashikamanisha nami watu wa Israeli na watu wa Yuda, ili wajulikane kwa jina langu, wanisifu na kunitukuza. Lakini wao hawakunisikiliza. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”

12. Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli, aliniambia hivi: “Waambie watu wa Israeli kwamba kila mtungi utajazwa divai. Lakini utakapowaambia hivyo, wao watakujibu hivi: ‘Kwani unadhani sisi hatujui kwamba kila mtungi utajazwa divai?’

13. Nawe utawaambia kuwa mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Nitawalewesha wenyeji wote wa nchi hii; wafalme wanaotawala mahali pa Daudi, makuhani, manabii na wakazi wote wa Yerusalemu.

14. Nitawagonganisha wao kwa wao kina baba na watoto. Sitawahurumia, sitawaachia wala sitawarehemu, bali nitawaangamiza.”

15. Enyi Waisraeli, sikilizeni kwa makini,msiwe na majivuno maana Mwenyezi-Mungu anasema nanyi.

16. Mtukuzeni Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu,kabla hajawaletea giza,nanyi mkajikwaa miguu kwenye milima ya giza.Nyinyi mnatazamia mwanga,lakini anaugeuza kuwa utusitusina kuufanya kuwa giza nene.

17. Lakini kama msiponisikiliza,moyo wangu utalia machozi faraghani,kwa sababu ya kiburi chenu.Nitalia kwa uchungu na kububujika machozi,kwa kuwa watu wa Mwenyezi-Mungu wametekwa.

18. Mwambie mfalme na mama yake hivi:“Shukeni kwenye viti vyenu vya enzi,maana taji zenu nzuri zimeanguka vichwani mwenu.

19. Miji ya Negebu imezingirwa;hakuna awezaye kufungua malango yake.Watu wa Yuda wamechukuliwa mateka,wote kabisa wamepelekwa utumwani.”

20. Inua macho yako, ee Yerusalemu!Tazama! Madui zako waja kutoka kaskazini.Kundi ulilokabidhiwa liko wapi?Kundi lako zuri li wapi?

21. Utasemaje juu ya wale uliodhani ni rafiki,wale ambao wewe mwenyewe uliwafundisha,watakapokushinda na kukutawala?Je, si utakumbwa na uchungukama wa mama anayejifungua?

22. Nawe utajiuliza moyoni mwako,“Kwa nini mambo haya yamenipata?”Sawa! Kama vazi lako limepandishwa juu,nawe ukatendewa kwa ukatili mno,hayo ni matokeo ya makosa yako mengi mno.

23. Je, Mwethiopia aweza kubadili rangi yake,au chui madoadoa yake?Ikiwezekana, nanyi pia mnaweza kutenda mema,nyinyi mliozoea kutenda maovu!

Kusoma sura kamili Yeremia 13