Agano la Kale

Agano Jipya

Wimbo Ulio Bora 2:1-6 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mimi ni ua la Sharoni,ni yungiyungi ya bondeni.

2. Kama yungiyungi kati ya michongoma,ndivyo alivyo mpenzi wangu kati ya wasichana.

3. Kama mtofaa kati ya miti ya msituni,ndivyo alivyo mpenzi wangu kati ya wavulana.Nafurahia kuketi chini ya kivuli chake,na tunda lake tamu sana kwangu.

4. Alinichukua hadi ukumbi wa karamu,akatweka bendera ya mapenzi juu yangu.

5. Nishibishe na zabibu kavu,niburudishe kwa matofaa,maana naugua kwa mapenzi!

6. Mkono wake wa kushoto chini ya kichwa changu,mkono wake wa kulia wanikumbatia.

Kusoma sura kamili Wimbo Ulio Bora 2