Agano la Kale

Agano Jipya

Waamuzi 5:17-31 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Kabila la Gileadi lilibaki ngambo ya Yordani.Kabila la Dani, kwa nini mlibaki merikebuni?Kabila la Asheri lilitulia huko pwani ya bahari,lilikaa bandarini mwake.

18. Watu wa Zebuluni ni watuwaliohatarisha maisha yao katika kifo.Hata wa Naftali walikikabili kifokwenye miinuko ya mashamba.

19. “Huko Taanaki, kando ya chemchemi za Megido,wafalme walikuja, wakapigana;wafalme wa Kanaani walipigana,lakini hawakupata nyara za fedha.

20. Nyota kutoka mbinguni zilishiriki vita,zilifuata njia zao, zilipigana na Sisera.

21. Mafuriko ya mto Kishoni yaliwachukua mbali,naam, mafuriko makali ya mto Kishoni.Songa mbele kwa nguvu, ee nafsi yangu!

22. “Farasi walipita wakipiga shoti;,walikwenda shoti na kishindo cha kwato zao.

23. Malaika wa Mwenyezi-Mungu asema hivi:‘Uapizeni mji wa Merosi,waapizeni vikali wakazi wake;maana hawakuja kumsaidia Mwenyezi-Munguhawakumsaidia Mwenyezi-Mungu dhidi ya wenye nguvu’.

24. “Abarikiwe kuliko wanawake woteYaeli, mke wa Heberi, Mkeni.Naam, amebarikiwa kuliko wanawake wotewanaokaa mahemani.

25. Sisera alimwomba maji, naye akampa maziwa;alimletea siagi katika bakuli ya heshima.

26. Kwa mkono mmoja alishika kigingi cha hema,na kwa mkono wake wa kulia nyundo ya fundi;alimponda Sisera kichwa,alivunja na kupasuapasua paji lake.

27. Sisera aliinama, akaanguka;alilala kimya miguuni pake.Hapo alipoinama ndipo alipoanguka, amekufa!

28. “Mama yake Sisera alitazama dirishanialichungulia katika viunzi vyake, akalalamika:‘Kwa nini gari lake limechelewa?Mbona vishindo vya magari yake vimechelewa kusikika?’

29. Jibu akalipata kwa wanawake wenye hekima:Akajituliza tena na tena kwa jibu hilo:

30. ‘Bila shaka wanatafuta na kugawana nyara;msichana mmoja au wawili kwa kila askari,vazi la sufu ya rangi kwa ajili ya Sisera.Vazi la sufu iliyotariziwa,na mikufu miwili ya nakshi kwa ajili ya shingo yangu!’

31. “Ee Mwenyezi-Mungu, waangamie adui zako wote!Lakini rafiki zako na wawe kama jua,wakati linapochomoza kwa mwanga mkubwa!”Nayo nchi ikawa na amani kwa muda wa miaka arubaini.

Kusoma sura kamili Waamuzi 5