Agano la Kale

Agano Jipya

Waamuzi 14:14-17 Biblia Habari Njema (BHN)

14. Nao wakamwambia, “Haya tega tusikie.” Samsoni akawaambia,“Kwa mla kukatoka mlokwa mwenye nguvu, utamu.”Baada ya siku tatu hao vijana walikuwa bado hawajaweza kutegua hicho kitendawili.

15. Basi siku ya saba wakamwambia mke wa Samsoni, “Mbembeleze mumeo ili atuambie maana ya kitendawili hicho, la sivyo tutakuteketeza kwa moto wewe pamoja na nyumba ya baba yako. Je, mlitualika hapa kuja kutunyanganya mali zetu?”

16. Mke wa Samsoni akamwendea Samsoni, huku machozi yanamtiririka, akamwambia, “Kwa kweli unanichukia; hunipendi hata kidogo. Umewategea kitendawili watu wangu na hukuniambia maana yake.”Samsoni akamjibu, “Mimi sijawaeleza hata wazazi wangu. Sasa nitawezaje kukuambia wewe?”

17. Lakini aliendelea kulia katika muda wao wote wa siku saba za sherehe za harusi. Siku ya saba Samsoni akamwambia mkewe kile kitendawili kwani alimbana sana. Mkewe akaenda haraka akawaambia watu wake.

Kusoma sura kamili Waamuzi 14