Agano la Kale

Agano Jipya

Sefania 3:11-20 Biblia Habari Njema (BHN)

11. “Siku hiyo, haitakulazimu kuona aibu,kutokana na matendo yako ya kuniasi,maana nitawaondoa miongoni mwakowale wanaojigamba na kujitukuzanawe hutakuwa na kiburi tena katika mlima wangu mtakatifu.

12. Nitakuachia watu wapole na wanyenyekevuambao watakimbilia usalama kwangu mimi Mwenyezi-Mungu.

13. Waisraeli watakaobaki,hawatatenda mabaya wala hawatasema uongo;wala kwao hatapatikana mdanganyifu yeyote.Watapata malisho na kulalawala hakuna mtu atakayewatisha.”

14. Imba kwa sauti, ewe Siyoni,paza sauti ee Israeli.Furahi na kushangilia kwa moyo wote, ewe Yerusalemu!

15. Mwenyezi-Mungu amekuondolea hukumu iliyokukabili,amewageuzia mbali adui zako.Mwenyezi-Mungu, mfalme wa Israeli yuko pamoja nawehutaogopa tena maafa.

16. Siku hiyo, mji wa Yerusalemu utaambiwa:“Usiogope, ee Siyoni,usilegee mikono.

17. Mwenyezi-Mungu, Mungu wako yu pamoja naweyeye ni shujaa anayekuletea ushindi.Yeye atakufurahia kwa furaha kuu,kwa upendo wake atakujalia uhai mpya.Atakufurahia kwa wimbo wa sauti kubwa,

18. kama vile katika siku ya sikukuu.”Mwenyezi-Mungu asema:“Nitakuondolea maafa yako,nawe hutahitaji kuona aibu kwa ajili yake.

19. Wakati huo, nitawaadhibu wote wanaokukandamiza.Nitawaokoa vilema na kuwakusanya waliotupwa,na kubadili aibu yao kuwa sifana fahari duniani kote.

20. Wakati huo nitawakusanya,na kuwafanya mjulikane na kusifiwa,miongoni mwa watu wote dunianinitakapowarudishia hali yenu njemananyi muone kwa macho yenu wenyewe.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”

Kusoma sura kamili Sefania 3