Agano la Kale

Agano Jipya

Nehemia 9:16-30 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Lakini wao na babu zetu wakawa na kiburina wakawa na shingo ngumuwakakataa kufuata maagizo yako.

17. Wakakataa kutii;wasiyakumbuke maajabu uliyofanya miongoni mwao.Wakawa na shingo zao ngumu,wakajichagulia kiongozi wa kuwarudishautumwani nchini Misri.Bali wewe Mungu u mwepesi kusamehe,mwenye neema na huruma,wewe hukasiriki upesi.U mwenye fadhili nyingi, na hukuwatupa.

18. Hata walipojitengenezea sanamu ya ndama na kusema,‘Huyu ndiye mungu wetualiyetutoa kutoka nchi ya Misri,’wakawa wamefanya kufuru kubwa.

19. Wewe kwa huruma zako nyingihukuwatupa kule jangwani.Mnara wa winguuliowaongoza mchana haukuondoka,wala mnara wa motouliowamulikia njia usiku, haukuondoka.

20. Ukawapa roho yako njema kuwashauri;ukawapa mana kuwa chakula chao na maji ya kunywaili kutuliza kiu chao.

21. Ukawatunza jangwani kwa miaka arubainina hawakukosa chochote;mavazi yao hayakuchakaawala nyayo zao hazikuvimba.

22. “Ukawaruhusu kushinda falme na mataifa,ukawafanyia mengi kila upande.Wakaishinda nchi ya Heshbonialikotawala mfalme Sihoni;na tena wakaishinda nchi ya Bashanialikotawala mfalme Ogu.

23. Wazawa wao ukawafanya wawe wengikama nyota za mbinguni;ukawaleta katika nchiuliyowaahidi babu zao.

24. Hivyo, hao wazawa wakaja na kuimiliki nchi;uliwashinda wakazi wa nchi hiyo,Wakanaani, ukawatia mikononi mwao,pamoja na wafalme wao,watu wao na nchi yao ili wawatende wapendavyo.

25. Miji yenye ngome wakaiteka,wakachukua nchi yenye utajiri,majumba yenye vitu vingi vizuri,visima vilivyochimbwa,mashamba ya mizabibu na mizeitunipamoja na miti yenye matunda kwa wingi.Hivyo wakala,wakashiba na kunenepana kuufurahia wema wako.

26. Lakini hawakuwa waaminifu kwako.Wakakuasi,wakaiacha sheria yakona kuwaua manabii waliowaonyaili wakurudie wewe.Wakakufuru sana.

27. Hivyo, ukawatia katika mikono ya adui zao,nao wakawatesa.Lakini wakiwa katika mateso yao,wakakulilia, nawe ukawasikia kutoka mbinguni.Na kwa huruma zako nyingi,ukawapelekea viongozi wa kuwaokoa;nao wakawakomboa toka mikononi mwao.

28. Lakini amani ilipopatikanawakatenda dhambi tena mbele yako,nawe ukawaacha watiwe katikamikono ya adui zao wawatawale.Hata hivyo, walipotubu na kukuliliaukawasikiliza kutoka mbinguni.Na kwa kulingana na huruma zako nyingi,ukawaokoa mara nyingi.

29. Ukawaonya ili wairudie sheria yako.Hata hivyo, kwa kiburi chao,wakaacha kuzitii amri zako.Wakayaasi maagizo yako,ambayo kwayo mtu akiyatii, ataishi.Wakawa wajeuripia wakafanya shingo zao ngumu,na wakakataa kuwa watiifu.

30. Ukawavumilia kwa miaka mingi,na kuwaonya kwa njia ya roho yakokwa kupitia manabii wako;hata hivyo hawakusikiliza.Basi ukawaachaukawatia mikononi mwa mataifa mengine.

Kusoma sura kamili Nehemia 9