Agano la Kale

Agano Jipya

Mika 5:8-15 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Wazawa wa Yakobo watakaobaki hai,wameenea miongoni mwa mataifa na watu wengiwatakuwa na nguvu kubwakama simba kati ya wanyama wa porini,kama mwanasimba miongoni mwa makundi ya kondoo,ambaye kila mahali apitapo,huyarukia na kuyararua mawindo yake,asiwepo mtu yeyote wa kuyaokoa.

9. Waisraeli watawashinda adui zaona kuwaangamiza kabisa.

10. Mwenyezi-Mungu asema,“Wakati huo nitawaondoa farasi wenu,na kuyaharibu magari yenu ya farasi.

11. Nitaiharibu miji ya nchi yenu,na kuzibomolea mbali ngome zenu.

12. Nitatokomeza matendo yenu ya uchawi,nanyi hamtakuwa tena na wapiga ramli.

13. Nitaziharibu sanamu zenu,na nguzo zenu za ibada;nanyi mtakoma kuabudu vitu mlivyotengeneza wenyewe.

14. Nitazing'oa sanamu za Ashera kutoka kwenu,na kuiangamiza miji yenu.

15. Kwa hasira na ghadhabu yangu,nitalipiza kisasi mataifa yote yasiyonitii.”

Kusoma sura kamili Mika 5