1. Ole wao wanaopanga kutenda maovuwanaolala usiku wakiazimia uovu!Mara tu kunapopambazuka,wanayatekeleza kwani wanao uwezo.
2. Hutamani mashamba na kuyatwaa;wakitaka nyumba, wananyakua.Huwadhulumu wenye nyumba na jamaa zao,huwanyang'anya watu mali zao.
3. Kwa hiyo, Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Ninapanga kuwaleteeni nyinyi maafa,ambayo kamwe hamtaweza kuyakwepa.Utakuwa wakati mbaya kwenu,wala hamtaweza kwenda kwa maringo.
4. Siku hiyo watu watawasimanga kwa wimbo,watalia na kuomboleza kwa uchungu, wakisema:‘Tumeangamia kabisa;Mwenyezi-Mungu amechukua nchi yetu,naam, ameiondoa mikononi mwetu.Mashamba yetu amewagawia waliotuteka.’”
5. Kwa hiyo hamtagawiwa sehemu yoyote ya ardhimiongoni mwa watu wake Mwenyezi-Mungu.
6. “Usituhubirie sisi.Mambo kama hayo si ya kuhubiriwa.Sisi hatutakumbwa na maafa!
7. Je, yafaa kusema hivyo, wazawa wa Yakobo?Je, Mwenyezi-Mungu ameacha uvumilivu wake?Je, yeye hufanya mambo kama haya?”Sivyo! Maneno yangu huwafaa watendao mambo mema.