Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 66:13-24 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Kama mama amtulizavyo mwanawe,kadhalika nami nitawatuliza;mtatulizwa mjini Yerusalemu.

14. Mtayaona hayo na mioyo yenu itafurahi;mifupa yenu itapata nguvu kama majani mabichi.Hapo itajulikana kuwa mimi Mwenyezi-Mungu huwalinda watumishi wangu,lakini nikikasirika huwaadhibu maadui zangu.”

15. Mwenyezi-Mungu atakuja kama moto,na magari yake ya vita ni kimbunga.Ataiacha hasira yake ifanye kazi yake kwa ukali,na onyo lake litekelezwe kwa miali ya moto.

16. Mwenyezi-Mungu atatoa hukumu kwa moto,atawaadhibu watu wote kwa upanga;nao atakaowaangamiza watakuwa wengi.

17. Mwenyezi-Mungu asema hivi: “Wapo watu wanaojitakasa na kutawadha wapate kuingia kwenye bustani za ibada za sanamu; wanafanya maandamano na kuhani akiwa kati yao. Watu hao hula nguruwe, panya na vyakula vingine haramu. Watu hao hakika watakufa wote pamoja.

18. Nayajua matendo yao na mawazo yao. Naja kuwakusanya watu wa mataifa yote na lugha zote, wajumuike pamoja na kuuona utukufu wangu.

19. Nitaweka kati yao alama ya uwezo wangu. Watakaosalimika kati yao nitawapeleka kwa watu wa mataifa huko Tarshishi, Puti, Ludi, nchi zenye wapiga upinde stadi; watakwenda pia Tubali na Yowani na nchi ambapo watu hawajapata kusikia umaarufu wangu wala kuuona utukufu wangu. Hao wajumbe wangu watautangaza utukufu wangu katika mataifa hayo.

20. Watawarejesha ndugu zenu wote kutoka katika mataifa yote kama matoleo yangu mimi Mwenyezi-Mungu. Watawaleta wamepanda farasi, nyumbu, ngamia na magari ya farasi mpaka Yerusalemu, kwenye mlima wangu mtakatifu. Watawaleta kama Waisraeli waletavyo sadaka ya nafaka katika chombo safi hadi nyumbani kwangu mimi Mwenyezi-Mungu.

21. Pia nitawachagua baadhi yao kuwa makuhani na baadhi yao kuwa Walawi. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

22. “Kama vile mbingu mpya na dunia mpya nitakazoumbazitakavyodumu milele kwa uwezo wangu,ndivyo wazawa wako na jina lako litakavyodumu.

23. Katika kila sikukuu ya mwezi mpya,na katika kila siku ya Sabato,binadamu wote watakuja kuniabudu.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

24. “Kisha watakwenda kuziona maiti za wale walioniasi. Wadudu watakaowala hawatakufa, na moto utakaowachoma hautazimika kamwe. Watakuwa chukizo kwa watu wote.”

Kusoma sura kamili Isaya 66