Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 49:8-24 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Wakati wa kufaa nilikujibu ombi lako;wakati wa wokovu nilikusaidia.Nimekuweka na kukufanyauwe kiungo cha agano langu na mataifa yote:Kuirekebisha nchi iliyoharibika,na kuwarudishia wenyewe ardhi hiyo;

9. kuwaambia wafungwa, ‘Tokeni humo gerezani’,na wale walio gizani, ‘Njoni nje mwangani!’Kila mahali watakapokwenda watapata chakulahata kwenye vilima vitupu watapata malisho.

10. Hawataona tena njaa wala kuwa na kiu.Upepo wa hari wala jua havitawachoma,mimi niliyewahurumia nitawaongozana kuwapeleka kwenye chemchemi za maji.

11. Milima yote nitaifanya kuwa njia,na barabara zangu kuu nitazitengeneza.

12. Watu wangu watarudi kutoka mbali,wengine kutoka kaskazini na magharibi,wengine kutoka upande wa kusini.”

13. Imbeni kwa furaha, enyi mbingu!Shangilia ewe dunia.Pazeni sauti mwimbe enyi milima,maana Mwenyezi-Mungu amewafariji watu wake,naam, atawaonea huruma watu wake wanaoteseka.

14. Wewe Siyoni wasema:“Mwenyezi-Mungu ameniacha;hakika Bwana wangu amenisahau.”

15. Lakini Mwenyezi-Mungu asema:“Je, mama aweza kumsahau mwanawe anayenyonya,asimwonee huruma mtoto wa tumbo lake?Hata kama mama aweza kumsahau mwanawe,mimi kamwe sitakusahau.

16. Nimekuchora katika viganja vyangu;kuta zako naziona daima mbele yangu.

17. Watakaokujenga upya wanakuja haraka,wale waliokuharibu wanaondoka.

18. Inua macho uangalie pande zote;watu wako wote wanakusanyika na kukujia.Naapa kwa nafsi yangu mimi Mwenyezi-Mungu,watu wako watakuwa kwako kama mapambo,utawafurahia kama afanyavyo bibi arusi na utaji wake.

19. “Kweli umekumbana na uharibifu,makao yako yamekuwa matupu,na nchi yako imeteketezwa.Lakini sasa itakuwa ndogo mno kwa wakazi wake;na wale waliokumaliza watakuwa mbali.

20. Wanao waliozaliwa uhamishoni,watakulalamikia wakisema:‘Nchi hii ni ndogo mno;tupatie nafasi zaidi ya kuishi.’

21. Hapo ndipo utakapojiuliza mwenyewe:‘Nani aliyenizalia watoto wote hawa?Nilifiwa na wanangu bila kupata wengine.Nilipelekwa uhamishoni na kutupwa mbali;nani basi aliyewalea watoto hawa?Mimi niliachwa peke yangu,sasa, hawa wametoka wapi?’”

22. Bwana Mungu asema hivi:“Nitayapungia mkono mataifa;naam, nitayapa ishara,nayo yatawabeba watoto wenu wa kiume,kadhalika na watoto wenu wa kikena kuwarudisha kwako.

23. Wafalme watakushughulikia,na malkia watakutengenezea chakula.Watakusujudia na kukupa heshima,na kuramba vumbi iliyo miguuni pako.Hapo utatambua kuwa mimi ni Mwenyezi-Mungu;wote wanaonitegemea hawataaibika.”

24. Watu wa Yerusalemu walalamika:“Je, shujaa aweza kunyanganywa nyara zake?Au mateka wa mtu katili waweza kuokolewa?”

Kusoma sura kamili Isaya 49