Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 49:7-14 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Mwenyezi-Mungu, Mkombozi na Mtakatifu wa Israeli,amwambia hivi yule anayedharauliwa mno,yule anayechukiwa na mataifa,na ambaye ni mtumishi wa watawala:“Wafalme watakuona nao watasimama kwa heshima,naam, wakuu watainama na kukusujudiakwa sababu yangu mimi Mwenyezi-Munguambaye hutimiza ahadi zangu;kwa sababu yangu mimi Mtakatifu wa Israeliambaye nimekuteua wewe.”

8. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Wakati wa kufaa nilikujibu ombi lako;wakati wa wokovu nilikusaidia.Nimekuweka na kukufanyauwe kiungo cha agano langu na mataifa yote:Kuirekebisha nchi iliyoharibika,na kuwarudishia wenyewe ardhi hiyo;

9. kuwaambia wafungwa, ‘Tokeni humo gerezani’,na wale walio gizani, ‘Njoni nje mwangani!’Kila mahali watakapokwenda watapata chakulahata kwenye vilima vitupu watapata malisho.

10. Hawataona tena njaa wala kuwa na kiu.Upepo wa hari wala jua havitawachoma,mimi niliyewahurumia nitawaongozana kuwapeleka kwenye chemchemi za maji.

11. Milima yote nitaifanya kuwa njia,na barabara zangu kuu nitazitengeneza.

12. Watu wangu watarudi kutoka mbali,wengine kutoka kaskazini na magharibi,wengine kutoka upande wa kusini.”

13. Imbeni kwa furaha, enyi mbingu!Shangilia ewe dunia.Pazeni sauti mwimbe enyi milima,maana Mwenyezi-Mungu amewafariji watu wake,naam, atawaonea huruma watu wake wanaoteseka.

14. Wewe Siyoni wasema:“Mwenyezi-Mungu ameniacha;hakika Bwana wangu amenisahau.”

Kusoma sura kamili Isaya 49