Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 46:8-13 Biblia Habari Njema (BHN)

8. “Kumbukeni jambo hili na kutafakari,liwazeni akilini mwenu enyi wakosefu.

9. Kumbukeni mambo niliyotenda hapo kale!Mimi ndimi Mungu na hakuna mwingine;naam, mimi ni Mungu, wala hakuna mwingine kama mimi.

10. Nilitangaza mambo ya mwisho tangu mwanzo,tangu kale nilitangaza mambo yatakayotukia.Lengo langu litatimia;mimi nitatekeleza nia yangu yote.

11. Ninamwita tai wangu kutoka mashariki,naam, msiri wangu kutoka nchi ya mbali.Mimi nimenena na nitayafanya;mimi nimepanga nami nitatekeleza.

12. “Nisikilizeni, enyi wenye vichwa vigumu,nisikilizeni enyi mlio mbali na ukombozi.

13. Siku ya kuwakomboa naileta karibu,haiko mbali tena;siku ya kuwaokoeni haitachelewa.Nitauokoa mji wa Siyoni,kwa ajili ya Israeli, fahari yangu.

Kusoma sura kamili Isaya 46