8. “Kumbukeni jambo hili na kutafakari,liwazeni akilini mwenu enyi wakosefu.
9. Kumbukeni mambo niliyotenda hapo kale!Mimi ndimi Mungu na hakuna mwingine;naam, mimi ni Mungu, wala hakuna mwingine kama mimi.
10. Nilitangaza mambo ya mwisho tangu mwanzo,tangu kale nilitangaza mambo yatakayotukia.Lengo langu litatimia;mimi nitatekeleza nia yangu yote.
11. Ninamwita tai wangu kutoka mashariki,naam, msiri wangu kutoka nchi ya mbali.Mimi nimenena na nitayafanya;mimi nimepanga nami nitatekeleza.
12. “Nisikilizeni, enyi wenye vichwa vigumu,nisikilizeni enyi mlio mbali na ukombozi.
13. Siku ya kuwakomboa naileta karibu,haiko mbali tena;siku ya kuwaokoeni haitachelewa.Nitauokoa mji wa Siyoni,kwa ajili ya Israeli, fahari yangu.