Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 45:11-24 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Mwenyezi-Mungu, Mtakatifu wa Israeli,Mungu, Muumba wa Israeli asema:“Je, mwathubutu kuniuliza juu ya watoto wangu,au kuniamuru juu ya kazi zangu mwenyewe?

12. Ni mimi niliyeifanya dunia,na kuumba binadamu aishiye humo.Mikono yangu ndiyo iliyozitandaza mbingu,na jeshi lote la nyota liko kwa amri yangu.

13. Ni mimi niliyemwamuru Koreshi kuchukua hatua,atekeleze matakwa yangu.Nitazifanikisha njia zake zote;ataujenga upya mji wangu Yerusalemu,na kuwapa uhuru watu wangu walio uhamishoni,bila kutaka malipo wala zawadi.”Mwenyezi-Mungu wa majeshi amesema.

14. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Utajiri wa Misri na bidhaa za Kushi,pamoja na za watu wa Seba, majitu marefu,zitakuja kwako mwenyewe wewe taifa la Israeli,zote zitakuwa mali yako.Watu hao watakutumikia wamefungwa minyororo;watakusujudia na kukiri wakisema:‘Kwako kuna Mungu wa kweli,wala hakuna Mungu mwingine ila yeye.’”

15. Kweli wewe ni Mungu uliyefichika,Mungu wa Israeli, Mungu Mwokozi.

16. Watengenezaji sanamu wataaibika na kufadhaika,wote kwa pamoja watavurugika.

17. Lakini taifa la Israeli litaokolewa na Mwenyezi-Mungu,litapata wokovu wa milele.Halitaaibishwa wala kufadhaishwa milele.

18. Mwenyezi-Mungu, Mungu pekee,ndiye aliyeiumba dunia,ndiye aliyeiumba na kuitegemeza.Hakuiumba iwe ghasia na tupu,ila aliiumba ikaliwe na viumbe vyake.Yeye asema sasa:“Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu,wala hakuna mwingine.

19. Mimi sikunena kwa siri,wala katika nchi yenye giza.Mimi sikuwaambia wazawa wa Yakobowanitafute katika ghasia.Mimi Mwenyezi-Mungu husema ukweli,maneno yangu ni ya kuaminika.”

20. Enyi watu wa mataifa mliosalia,kusanyikeni pamoja mje!Nyinyi mmekosa akili:Nyinyi mwabeba sanamu za mitina kumwomba mungu asiyeweza kuokoa watu.

21. Semeni wazi na kutoa hoja zenu;shaurianeni pamoja!Ni nani aliyetangaza zamani matukio ya sasa?Ni nani aliyetamka mambo haya zamani?Je, haikuwa mimi Mwenyezi-Mungu?Hakuna Mungu mwingine ila mimi!Mimi ni Mungu wa haki na mwokozi;hakuna mwingine ila mimi.

22. Nigeukieni mimi mpate kuokolewa,popote mlipo duniani.Maana mimi ni Mungu, wala hakuna mwingine.

23. Mimi nimeapa kwa nafsi yangu,ninachotamka ni ukweli,neno langu halitarudi nyuma:Kila binadamu atanipigia magoti,kila mtu ataapa uaminifu.

24. “Watasema juu yangu,‘Haki na nguvu viko kwa Mwenyezi-Mungu peke yake.’”Wote waliomwakia hasira Mwenyezi-Munguwatamjia yeye na kuaibishwa.

Kusoma sura kamili Isaya 45