Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 44:1-7 Biblia Habari Njema (BHN)

1. “Sikiliza ewe taifa Israeli mtumishi wangu;sikiliza ewe kizazi cha Yakobo mteule wangu.

2. Mimi, Mwenyezi-Mungu Muumba wako,niliyekufanya tangu tumboni mwa mama yako,nimekuja kukusaidia wewe.Mimi Mwenyezi-Mungu nasema:Usiogope, ewe taifa la Yakobo, mtumishi wangu,naam, usiogope ewe Yeshuruni mteule wangu.

3. “Nitaimwagilia maji nchi iliyokauka,na kutiririsha mto katika nchi kame.Nitawamiminia roho yangu wazawa wako,nitawamwagia watoto wako baraka yangu.

4. Watachipua kama nyasi penye maji mengi,kama majani kandokando ya vijito.

5. “Mmoja atasema: ‘Mimi ni wa Mwenyezi-Mungu’,mwingine atajiita kwa jina la Yakobo,mwingine ataandika mkononi mwake, ‘Wa Mwenyezi-Mungu’,na kujitambulisha kwa jina la Israeli.”

6. Mwenyezi-Mungu, Mfalme na Mkombozi wa Israeli,naam, Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema hivi:“Mimi ni wa kwanza na wa mwisho;hakuna Mungu mwingine ila mimi.

7. Ni nani Mungu aliye kama mimi?Mwache atangaze na kusema wazi mbele yangu.Nani alitangaza hapo kale mambo ambayo yatatukia?Na watuambie yale ambayo bado kutokea.

Kusoma sura kamili Isaya 44