Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 41:21-26 Biblia Habari Njema (BHN)

21. Mwenyezi-Mungu, Mfalme wa Yakobo, asema:“Enyi miungu ya mataifa,njoni mtoe hoja zenu!

22. Leteni hoja zenu, mtuambie yatakayotukia.Tuambieni matukio ya kwanza yalikuwa yapinasi tutayatafakari moyoni.Au tutangazieni yajayo,tujue yatakayokuja.

23. Tuambieni yatakayotokea baadaye,nasi tujue basi kama nyinyi ni miungu.Fanyeni kitu chochote, chema au kibaya,ili tutishike na kuogopa.

24. Hakika, nyinyi si kitu kabisa.hamwezi kufanya chochote kile.Anayechagua kuwaabudu nyinyi ni chukizo.

25. “Nimechochea mtu toka kaskazini,naye amekuja;naam, nimemchagua mtu toka mashariki,naye atalitamka jina langu.Yeye atawakanyaga wafalme kama tope,kama vile mfinyanzi apondavyo udongo wake.

26. Nani aliyebashiri haya tangu mwanzo,hata sisi tupate kuyatambua?Nani aliyetangulia kuyatangaza,ili sasa tuseme, alisema ukweli?Hakuna hata mmoja wenu aliyeyataja,wala hakuna aliyesikia maneno yenu.

Kusoma sura kamili Isaya 41