Agano la Kale

Agano Jipya

Ezekieli 37:15-22 Biblia Habari Njema (BHN)

15. Neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia;

16. “Wewe mtu! Chukua kijiti kimoja, uandike juu yake maneno haya: ‘Kwa Yuda na Waisraeli wanaohusiana naye.’ Kisha chukua kijiti kingine, uandike juu yake maneno haya: ‘Kwa Yosefu (kijiti cha Efraimu) na Waisraeli wanaohusiana naye.’

17. Halafu vichukue vijiti hivyo na kuvishikamanisha ili vionekane kama kijiti kimoja.

18. Wananchi wenzako watakapouliza, ‘Je, hutatueleza maana ya jambo hilo?’

19. Wewe utawajibu, Bwana Mwenyezi-Mungu asema hivi: Nitakitwaa kijiti cha Yosefu (kilichomo mkononi mwa Efraimu) na makabila ya Israeli yanayounganika naye, nami nitakishikamanisha na kijiti cha Yuda ili vijiti hivyo viwili vifanywe kijiti kimoja mkononi mwangu.

20. “Ukiwa mbele yao huku umeshika vijiti ulivyoandika juu yake,

21. waambie kuwa mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Nitawatoa Waisraeli kutoka mataifa walikokwenda; nitawakusanya toka pande zote na kuwarudisha katika nchi yao.

22. Nitawafanya kuwa taifa moja katika nchi juu ya milima ya Israeli; mfalme mmoja atakuwa mfalme wao wote. Hawatakuwa tena mataifa mawili wala hawatagawanyika tena kuwa falme mbili.

Kusoma sura kamili Ezekieli 37