Agano la Kale

Agano Jipya

Ezekieli 30:7-15 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Misri itakuwa jangwa kama nchi zilizo jangwana miji yake itakuwa magofu kama miji iliyoteketezwa.

8. Nitakapoiteketeza Misri kwa motona kuwavunjilia mbali wasaidizi wake wotendipo watakapotambua kuwa mimi ni Mwenyezi-Mungu.

9. Siku hiyo, nitapeleka wajumbe kwenda kuwatishaWaethiopia wanaojidhani kuwa salama.Watatetemeka siku Misri itakapoangamia.Naam! Kweli siku hiyo yaja!

10. “Mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi:Nitamtumia Nebukadneza, mfalme wa Babuloni,kukomesha utajiri wa nchi ya Misri.

11. Nebukadneza mwenyewe pamoja na watu wake,taifa katili kuliko mataifa yote,watatumwa kuiangamiza nchi ya Misri.Watachomoa panga zao dhidi ya Misrina kuijaza nchi hiyo watu waliouawa.

12. Nitaukausha mto Nili na vijito vyake,na kuwauzia watu waovu nchi ya Misri.Nitasababisha uharibifu nchini kotekwa mkono wa watu wageni.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

13. “Mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi:Nitaharibu vinyago vya miungu,na kukomesha sanamu mjini Memfisi.Hakutakuwa na mkuu tena huko Misri.Nitasababisha hofu itawale nchini Misri.

14. Mji wa Pathrosi nitaufanya kuwa mtupu,mji wa Soani nitauwasha moto,mji wa Thebesi nitauadhibu.

15. Nitamwaga ghadhabu yangu juu ya Pelusiumu,ile ngome inayotegemewa na Misri;na kuangamiza makundi ya Thebesi.

Kusoma sura kamili Ezekieli 30