Agano la Kale

Agano Jipya

Danieli 6:17-20 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Jiwe likaletwa na kuwekwa mlangoni mwa lile pango. Mfalme akalipiga mhuri wake binafsi na ule wa wakuu wake, ili uamuzi kuhusu Danieli usibatilishwe.

18. Kisha mfalme akarudi katika ikuluni yake ambamo alikesha akifunga; hakufanya tafrija ya aina yoyote, na usingizi ukampaa.

19. Alfajiri na mapema, mfalme Dario aliamka, akaenda kwa haraka kwenye pango la simba.

20. Alipofika karibu akamwita Danieli kwa sauti ya huzuni, “Danieli, mtumishi wa Mungu aliye hai! Je, Mungu wako unayemtumikia daima ameweza kukuokoa na simba hawa?”

Kusoma sura kamili Danieli 6