Agano la Kale

Agano Jipya

Danieli 10:1-3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mnamo mwaka wa tatu wa utawala wa mfalme Koreshi wa Persia, Danieli, aliyeitwa pia Belteshaza, alipewa ufunuo. Ufunuo huo ulikuwa wa kweli, lakini ulikuwa mgumu sana, haukueleweka. Hata hivyo alielewa ufunuo huo maana pia alifahamu maono.

2. “Wakati huo, mimi Danieli, nilikuwa nikiomboleza kwa muda wa majuma matatu.

3. Sikula chakula cha fahari, sikugusa nyama wala divai, na sikujipaka mafuta kwa muda wa majuma hayo yote matatu.

Kusoma sura kamili Danieli 10