Agano la Kale

Agano Jipya

2 Wafalme 7:11-13 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Walinda malango wakaeneza habari hizi mpaka zikafika nyumbani kwa mfalme.

12. Ingawa kulikuwa bado giza, mfalme aliamka na kuwaambia maofisa wake, “Mimi najua mpango wa Waaramu! Wanajua tuna njaa mjini, sasa wameacha kambi yao kwenda kujificha ili tutakapokwenda kutafuta chakula, watukamate sote hai na kuuteka mji.”

13. Mmoja kati ya maofisa wake akasema, “Watu wengi tayari wameangamia kama vile wale ambao wamekwisha fariki. Tafadhali utume watu wachache na farasi watano wa wale waliobaki ili waende kuona kumetokea nini.”

Kusoma sura kamili 2 Wafalme 7