Agano la Kale

Agano Jipya

2 Mambo Ya Nyakati 20:32-36 Biblia Habari Njema (BHN)

32. Alitenda mema mbele ya Mwenyezi-Mungu kama alivyofanya Asa baba yake.

33. Lakini hakupaharibu mahali pa kutolea tambiko kilimani. Watu walikuwa bado hawajamgeukia na kumwabudu Mungu wa babu zao kwa mioyo yao.

34. Matendo mengine ya Yehoshafati, kutoka mwanzo wa utawala wake mpaka mwisho, yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za Yehu mwana wa Hanani, ambamo zimo katika kitabu cha Wafalme wa Israeli.

35. Baada ya haya, Yehoshafati mfalme wa Yuda, alijiunga na Ahazia mfalme wa Israeli, aliyetenda mambo maovu.

36. Walishirikiana kuunda merikebu za kusafiria mpaka Tarshishi; waliziundia huko Esion-geberi.

Kusoma sura kamili 2 Mambo Ya Nyakati 20