Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 12:6-20 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Elkana, Ishia, Azareli, Yoezeri, Yashobeamu kutoka ukoo wa Kora

7. na Yoela na Zebadia, wana wa Yerohamu, kutoka Gedori.

8. Tena, watu kutoka kabila la Gadi walijiunga na Daudi akiwa ngomeni kule nyikani. Hawa walikuwa askari wenye nguvu na uzoefu, hodari wa kutumia ngao na mkuki; wenye nyuso za kutisha kama simba na wepesi kama swala milimani.

9. Kiongozi wao mkuu alikuwa Ezeri, wa pili Obadia, wa tatu Eliabu,

10. wa nne Mishmana, wa tano Yeremia,

11. wa sita Atai, wa saba Elieli,

12. wa nane Yohanani, wa tisa Elsabadi,

13. wa kumi Yeremia, na wa kumi na moja Makbanai.

14. Wagadi hao, walikuwa maofisa wa jeshi. Kulingana na vyeo vyao, mdogo alisimamia kikosi cha wanajeshi 100, na mkubwa alisimamia kikosi cha wanajeshi 1,000.

15. Hawa ndio watu waliovuka mto Yordani mnamo mwezi wa kwanza, mto ulipokuwa umefurika pande zote na kuwatawanya watu mashariki na magharibi ya mto.

16. Baadhi ya watu kutoka makabila ya Benyamini na Yuda walifika ngomeni alipokuwa Daudi.

17. Daudi akatoka nje kuwalaki, akawaambia, “Ikiwa mmekuja kwangu kama marafiki ili kunisaidia basi nawapokea kwa moyo wote, lakini kama mmekuja ili kunisaliti kwa maadui zangu, ingawa sijatenda ovu lolote, Mungu wa baba zetu awaone na awakemee.”

18. Hapo Roho akamjia Abishai, mkuu wa hao watu thelathini, naye akasema,“Sisi tu watu wako, ee Daudi,tuko upande wako, ee mwana wa Yese!Amani, amani iwe kwako,na amani iwe kwa yeyote akusaidiaye!Maana akusaidiaye ndiye Mungu wako.”Ndipo Daudi akawapokea na kuwafanya maofisa katika jeshi lake.

19. Askari wengine wa kabila la Manase, walitoroka na kujiunga na Daudi, wakati alipoondoka pamoja na Wafilisti kwenda kupigana na mfalme Shauli. (Lakini hata hivyo, hakuwasaidia maana watawala wa Wafilisti walifanya shauri wamfukuze arudi Siklagi wakisema, “Tutayahatarisha maisha yetu kwa sababu atatutoroka arudi kwa bwana wake Shauli.”)

20. Basi, Daudi alipokuwa Siklagi, watu wafuatao wa kabila la Manase walimwendea: Adna, Yozabadi, Yediaeli, Mikaeli, Yozabadi, Elihu na Silethai. Kila mmoja wao alikuwa kiongozi wa kikosi cha watu 1,000 katika kabila la Manase.

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 12