Agano la Kale

Agano Jipya

Waroma 4:1-10 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Tuseme nini basi, juu ya Abrahamu baba yetu?

2. Kama Abrahamu alikuwa amefanywa mwadilifu kutokana na bidii yake, basi, anacho kitu cha kujivunia mbele ya Mungu.

3. Kwa maana, Maandiko Matakatifu yasema: “Abrahamu alimwamini Mungu, naye Mungu akamkubali kuwa mwadilifu.”

4. Mfanyakazi hulipwa mshahara; mshahara wake si zawadi bali ni haki yake.

5. Lakini mtu asiyetegemea matendo yake mwenyewe, bali anamwamini Mungu ambaye huwasamehe waovu, basi, Mungu huijali imani ya mtu huyo, akamkubali kuwa mwadilifu.

6. Naye Daudi asema hivi juu ya furaha ya mtu yule ambaye Mungu amemkubali kuwa mwadilifu bila kuyajali matendo yake:

7. “Heri wale waliosamehewa makosa yaoambao makosa yao yamefutwa.

8. Heri mtu yule ambayeBwana hataziweka dhambi zake katika kumbukumbu.”

9. Je, hiyo ni kwa wale waliotahiriwa tu, ama pia kwa wale wasiotahiriwa? Ni kwa wale wasiotahiriwa pia. Kwa maana tumekwisha sema: “Abrahamu aliamini, naye Mungu akamkubali kuwa mwadilifu.”

10. Je, Abrahamu alikubaliwa kabla ya kutahiriwa, ama baada ya kutahiriwa? Kabla ya kutahiriwa, na si baada ya kutahiriwa.

Kusoma sura kamili Waroma 4