Agano la Kale

Agano Jipya

Ufunuo 2:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. “Kwa malaika wa kanisa la Efeso andika: “Mimi nishikaye zile nyota saba katika mkono wangu wa kulia na ambaye hutembea katikati ya vinara saba vya taa vya dhahabu, nasema hivi:

2. Najua mambo yako yote; najua bidii yako na uvumilivu wako. Najua kwamba huwezi kuwavumilia watu waovu, na kwamba umewapima wale wanaojisemea kuwa mitume na kumbe sio, ukagundua kwamba ni waongo.

3. Wewe unayo saburi, umestahimili taabu nyingi kwa ajili ya jina langu, wala hukuvunjika moyo.

4. Lakini ninalo jambo moja dhidi yako: Wewe hunipendi tena sasa kama pale awali.

Kusoma sura kamili Ufunuo 2