Agano la Kale

Agano Jipya

Matendo 8:28-35 Biblia Habari Njema (BHN)

28. Alipokuwa anasafiri, alikuwa akijisomea kitabu cha nabii Isaya.

29. Basi, Roho Mtakatifu akamwambia Filipo, “Nenda karibu na gari hilo ukafuatane nalo.”

30. Filipo akakimbilia karibu na gari, akamsikia huyo mtu akisoma katika kitabu cha nabii Isaya. Hapo Filipo akamwuliza, “Je, unaelewa hayo unayosoma?”

31. Huyo mtu akamjibu, “Ninawezaje kuelewa bila mtu kuniongoza?” Hapo akamwalika Filipo apande juu, aketi pamoja naye.

32. Basi, sehemu ya Maandiko Matakatifu aliyokuwa anasoma ilikuwa hii:“Alikuwa kama kondoo anayepelekwa kuchinjwa;kimya kama vile mwanakondoo anapokatwa manyoya,yeye hakutoa sauti hata kidogo.

33. Alifedheheshwa na kunyimwa haki.Hakuna atakayeweza kuongea juu ya kizazi chake,kwa maana maisha yake yameondolewa duniani.”

34. Huyo Mwethiopia akamwambia Filipo, “Niambie, huyu nabii anasema juu ya nini? Anasema mambo haya juu yake yeye mwenyewe au juu ya mtu mwingine?”

35. Basi, Filipo akianzia na sehemu hiyo ya Maandiko Matakatifu, akamweleza Habari Njema juu ya Yesu.

Kusoma sura kamili Matendo 8